Ali Saleh Kiba al maarufu kama Alikiba ni miongoni mwa wasanii 
wakongwe na wakubwa Tanzania, Afrika Mashariki na pengine Afrika kwa 
ujumla. Ni mshindi wa tuzo zaidi ya 14 kwa mwaka 2016 ikiwezo tunzo 
kubwa kabisa za MTV EMA kwa kipengele cha Best African Act. 
Kwa mafanikio makubwa aliyoyapata mwaka jana ikiwemo kupata mkataba 
mnono wa kampuni kubwa ya muziki duniani yaani Sony Music na kushinda 
tuzo zote hizo ndani ya mwaka 2016 ni wazi kabisa kuwa thamani ya 
Alikiba imepanda maradufu barani Afrika na pengine kila mfuatiliaji wa 
muziki Afrika angependa zaidi kumfahamu Alikiba, kufahamu kazi zake, ni 
wapi ametoka na wapi anakwenda. 
Sekeseke lilitokea mwaka jana kwenye show ya Mombasa rocks 
iliyofanyika mjini Mombasa, Kenya kati ya Wizkid na Alikiba ni moja kati
 ya mambo ambayo yalifanya jina la Alikiba lizungumzwe sana barani 
Afrika haswa Tanzania, Kenya na Nigeria ambapo mitandao mbalimbali ya 
Nigeria iliripoti kua Alikiba anatrend sana nchini Nigeria. 
Ushindi wa MTV EMA pia ambao awali alipewa Wizkid kabla 
haujatenguliwa na kupewa Alikiba ni mambo yaliyofanya apate attention 
zaidi kwenye soko la muziki barani Afrika. 
Kutrend ni kitu muhimu sana katika soko la muziki kwa sasa, wasanii 
wengi duniani kote hata mpaka Marekani wamekuwa wakitengeneza kiki kabla
 ya kuachia kazi zao mpya ili kupata attention. Nafahamu kuwa msanii 
Alikiba amekuwa sio muumini mzuri sana wa kiki, lakini kiki kama hizi 
ambazo zinajitengeneza zenyewe ni dhambi kubwa kuacha kuzitumia 
kibiashara sababu kuna wanaotamani kutrend hata kwa kutembea uchi lakini
 hawazipati. 
Mapema mwaka huu Alikiba alitangaza ratiba ya World Tour yake 
itakayoanzia South Africa kisha America na kumalizikia barani Ulaya. Kwa
 mujibu wa ratiba kutoka kwenye posters zake alizozipost Instagram Tour 
yake inaanza February mwaka huu. Hivyo mpaka ninaandika makala hii 
zimebaki siku tatu kufikia mwezi February. 
Kati ya sehemu ngumu sana kupenya kimuziki barani basi ni Afrika 
Kusini na hii imetokana na ‘wasauzi’ kuthamini sana muziki wao na 
haikushangaza licha ya jina kubwa alilojijengea Diamond Platnumz kwenye 
kiwanda cha muziki barani Africa aliwahi kaririwa akisema amefanya 
collaboration na AKA ili kupenyeza muziki wake África Kusini. 
Sasa wasiwasi wangu ni je?  Alikiba anategemea kujaza viti kwa 
kuitegemea nyimbo ya Aje pekee?  Target yake kwenye hii tour ni kuifanya
 iwe ya kidunia au analenga waTanzania pekee wanaoishi kwenye nchi 
husika? Aliahidi atatoa Aje remix ambayo ni nyimbo aliyoimba na msanii 
kutoka Nigeria MI Abaga lakini mpaka zimebaki siku tatu kabla 
hatujaingia mwezi anaoanza tour hakuna dalili ya hiyo nyimbo?  
Binafsi nilidhani ingekuWa sahihi sana kama angeachia nyimbo ambayo 
amesharekodi mama mkongwe Yvonne Chakachaka kwa lengo la kuiteka zaidi 
South Africa kibiashara zaidi ili jina lake liwe kubwa nchini humo hata 
wakati wa Tour yake angetumia pia na fursa hiyo kufanya media tour 
kuitambulisha zaidi hiyo ngoma. 
Nadhani si Mimi ila asilimia 98 ya mashabiki hawaridhishwi na namna 
ambayo Alikiba amekuwa slow sana na kutojua namna soko la mUziki 
linavyoenda na nini linataka. Ni jana kupitia mtandao wa instagram 
msanii wa maigizo ambaye pia ni shabiki mkubwa wa msanii Alikiba alipost
 kipande cha screenshot kikionesha ujumbe aliotumiwa na shabiki mwingine
 wa Alikiba DM kua Ali atapoteza mashabiki wake sababu hawapi raha 
wanayoitaka,  siku zote amekuwa mtu wa kujiamini na kuwasibirisha 
mashabiki wake ambao ukweli bila wao asingekua hapo halipo leo. 
Mwaka mpya umeanza kwa kasi kweli kila mtu yuko kasi lakini naona Alikiba bado yule yule.