
Lowassa ambaye alitajwa na Profesa Lipumba kuwa chanzo cha yeye kujiuzulu kabla ya kurejea tena miezi tisa baadaye kutengua uamuzi wake, amesema kuwa kushindwa kwa chama hicho ni kushindwa kwao na vyama vyote vinavyounda UKAWA.
Mjumbe huyo alitumia ukurasa wake wa Facebook kueleza jinsi ambavyo Ukawa inalibeba tatizo la mgogoro unaendelea ndani ya chama cha CUF. “CUF ni wenzetu katika Ukawa. Shida zao ni shida zetu, vita vyao ni vita vyetu, kushindwa kwao ni kushindwa kwetu, ushindi wao ni ushindi wetu,” aliandika Lowassa.
Profesa Ibrahim Lipumba amekuwa akieleza kuwa hayuko tayari kuona Chadema au Lowassa wanakinunua chama hicho.
0 maoni: