
Pongezi hizo zilitolewa na Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Juma Simba, alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
“Rais Magufuli ameendesha vikao kwa muda mfupi, lakini kwa mafanikio makubwa na sisi kama CCM mkoa tutahakikisha tunashirikiana kwa karibu zaidi na viongozi wa taifa walioteuliwa hivi karibuni,” alisema Simba.
Aliongeza kuwa pamoja na Rais Magufuli kuendesha vikao hivyo kwa muda mfupi, lakini ameweza kutoa maamuzi mazito yenye lengo la kukijenga chama hicho kwa siku moja.
0 maoni: