Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Moses Nnauye
amekiri kuwepo kwa udhaifu katika sheria ambazo zinaliongoza Baraza la
Sanaa Taifa (BASATA) lililopewa dhamana ya kusimamia na stawisha
shughuli za sanaa nchini.
Waziri Nape
Waziri Nape amedai kwa sasa baraza hilo linakutana na wasanii wakati
wa kuzifungia kazi zao pale wanapokiuka maadili ya kazi za sanaa.
“BASATA ambalo ndio baraza lipo chini yangu sio rafiki kwa msanii,”
Waziri Nape alikiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM. “Msanii anakutana
na BASATA unapotakiwa kufungiwa wimbo wake au anapotakiwa kuonywa kwa
kupewa adhabu. Nataka sheria ilifikishe sehemu BASATA awe walezi wa
msanii. Sasa hivi wakiamua kuwa walezi akina Mngereza na wenzake ni kwa
mapenzi yao. Lakini nataka sheria iwalazishe wao sio polisi, wao ni
wazazi wanaotakiwa kulea na kuendeleza,”
Aliongeza, “Hata Bodi ya filamu wasionekane tu wakati wakufungiana,
waonekane pia wakati msanii anaanza kukua mpaka anafika mbali zaidi. Kwa
hiyo changamoto kubwa kwetu mfumo sio rafiki wa kuifanya sanaa yetu
itoke hapa iende mbele,”
Waziri huyo amesema serikali ikirekebisha sheria za sanaa na kuwa
rafiki kwa watumiaji anaamini sekta ya sanaa inaweza kutoa mchango
mkubwa katika kukuza pato la Taifa.
Saturday
RELATED STORIES
Kukamatwa kwa pombe za ‘viroba’ zasababisha mfanyabiashara ajiueOparesheni ya wafanyabiashara wa viroba inayoendelea nchini, imesababisha Mfanyabiashara mmoja aji
Tundu Lissu apandishwa kizimbaniMbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kis
Obama: Ningewania Urais ningeshinda, Trump amjibu!Rais wa Marekani anayemaliza muda wake, Barack Obama, amesema kama angekuwa anawania Urais mwaka h
Hili ni ombi la Rais Magufuli kwa Watanzania mwaka 2017Rais wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amewaomba Watanzania wote kuutunza na kuudumisha umoja k
kauli ya Zitto Kabwe baada ya uteuzi wa Anna MghwiraBaada ya uteuzi wa Rais Magufuli jana wa Mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo, Anna Mghwira kuwa
TID kumshtaki Steve Nyerere, ni baada ya kutuhumiwa kupokea milioni 2 za RC MakondaMsanii mkongwe wa muziki Khalid Mohamed ‘TID’ ameahidi kuwachukulia hatua watu wanaosambaza taarif
0 maoni: