Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Sunday

 kauli ya Zitto Kabwe baada ya uteuzi wa Anna Mghwira

kauli ya Zitto Kabwe baada ya uteuzi wa Anna Mghwira

Baada ya uteuzi wa Rais Magufuli jana wa Mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo, Anna Mghwira kuwa mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kulikuwa na mijadala mizito mitandaoni na hata kwenye vyombo vya habari juu ya uteuzi huo huku wengi wakimtaka Mbunge pekee wa chama hicho, Zitto Kabwe atolee ufafanuzi juu uteuzi huo hatimae leo ametoa kauli yake ya kwanza kuhusu uteuzi huo.
Tokeo la picha la zitto Kabwe na anna mghwira
Zitto Kabwe akiteta jambo na Mama Anna Mghwira
Zitto Kabwe amesema amezipokea taarifa hizo kutoka mitandaoni na kwenye vyombo vya habari lakini bado Chama cha ACT wazalendo hakijafanya mawasiliano na Mghwira anmbaye yupo nje ya nchi mpaka atakaporejea ndipo chama kitatoa msimamo wake juu ya uteuzi huo.
Nimekuwa naulizwa Sana kuhusu uteuzi wa Mwenyekiti wa Chama chetu kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Nimekuwa kimya Kwa sababu tumepokea Taarifa za uteuzi kutoka katika vyombo vya Habari. Mwenyekiti yuko nje ya nchi na kutokana na tofauti za masaa bado hatujawasiliana nae. Tutatoa tamko kamili atakapokuwa amerejea nchini.“ameandika Zitto Kabwe kwenye ukurasa wake wa Facebook.
Hata hivyo Zitto Kabwe amewataka Wanachama wa chama cha ACT wazalendo luwa watulivu kwa kipindi hiki mpaka hapo taarifa rasmi itakapotolewa pindi atakaporejea nchini.
Ninawataka wanachama wote wa Act Wazalendo wawe watulivu na Kama kuna masuala yanayohusu maamuzi ya vikao vya Chama tutawajulisha.“ameandika Zitto Kabwe.
Jobs at Musoma Water Supply and Sanitation Authority (MUWASA)

Jobs at Musoma Water Supply and Sanitation Authority (MUWASA)


VACANCIES
Musoma Water Supply and Sanitation Authority (MUWASA) is an utility established under section 9 of the Water Supply and Sanitation Act No. 12 of 2009 with the objective of provision of Water Supply and Sanitation services in Musoma Municipality. In this respect, the activities of MUWASA have specifically expanded and the authority now invites application from suitably qualified and skilled individuals who are dynamic and result oriented to fill the following posts:
0:1 Job Position: Information Technology Officer I (1 Post)
1 :1 Reporting to: Managing Director
1 :2 Duties and Responsibilities
i. To conduct system analysis related to computer applications.
ii. To design moderately complicated systems on the basis of systems analysis documents.
iii. To write detailed systems specifications related to moderately complicated applications.
iv. To conduct Systems analysis relating to computer applications.
v. To coordinate the data synchronization activities between the engineering and the billing departments.
vi. To manage the meter management billing system and data updating activities.
vii. To make regular back-ups to safeguard both Auto CAD and billing databases
viii. To performing any other duties that may be assigned by the Supervisor.
ix. To plan design and develop system related computer system and programming
1 :3 Minimum Qualifications
Holder of Bachelor Degree or Advanced Diploma in Computer Science, Computer Engineering, Information Communication Technology, Information Systems Analysis, Electronics and Communications from a recognized Institution,
1.4 Minimum Experience
Possession of at least Five (5) years of working in similar field.
1 :5 Age limit
Not above 45 years of age
===========
2:0 Job Position: Customer Relation Officer I 1 Post
2:1 Reporting to: Commercial Manager
2:2 Duties and Responsibilities
i. To identify customers and their needs.
ii. To prepare and develop market plans and programmes.
iii. To monitor and review business performance.
iv. To gather marketing information.
v.To process promotional materials as requested by departments and sections.
vi. To monitor sponsorship and donation requests.
vii. To monitor and maintain promotional materials.
viii. To maintain good customer service when dealing with internal and external customers.
ix. To follow up on supplies of promotional materials
x. To perform any other duties as may be assigned.
2:3 Minimum Qualifications
Holder of Bachelor Degree or Advanced Diploma qualifications in Marketing, Business Administration, Commerce, Mass Communication or related disciplines from recognized Institution, Possession of Master's Degree is an added advantage. He or She must be computer literate.
2.4 Minimum Experience
Possession of at least five (5) years of working in similar field.
2:5 Age limit
Not above 45 years of age
2:6 Remuneration
Active package and fringe benefits as per MUWASA's incentives scheme will be offered to the successful candidates.
Mode of Application
Only qualified persons should submit their handwritten letters of application with certified copies of relevant academic and professional certificates and testimonials so as to reach the undersigned not later than 21st June, 2017. Applicants are also required to indicate the names and contacts of at least three (3) work/professional related referees. Women are encouraged to apply. Only short listed candidates will be informed for interview.
The Managing Director
Musoma Water Supply and Sanitation Authority,
P. 0. Box 233,
MUSOMA.
NAFASI YA AJIRA TPC LIMITED, JUNE 2017

NAFASI YA AJIRA TPC LIMITED, JUNE 2017


VACANCY ANNOUNCEMENT
TPC Ltd is one of the fast growing sugar producing companies in Tanzania. The company is situated at the foot of Mount Kilimanjaro. 22 kms south of Moshi Municipality
Applications are invited from energetic, proactive and dynamic Tanzanians to fill vacant position in the Corporate Affairs Department.
POST: 1. RADIOGRAPHER(1Post)
1.0 Reports to the Hospital Manager
1.1 Core Job Description: To deal with day to day Radiographer duties and responsibilities.
1.2 Key Accountabilities
1.2.1 Preparing examination rooms, positioning patients for imaging exams.
1.2.2 Assessing and monitoring patients through treatment and follow-up.
1.2.3 Working closely with medical specialists to plan treatment of tissues defects.
1.2.4 Screening of abnormalities.
1.2.5 Producing and interpreting high quality images of the body to identify and diagnose injury and disease.
1.2.6 Asses patients and their requirements towork out which radiographic techniques to use.
1.2.7 Take responsibilities for radiation safety in your work area, including checking equipment for malfunctions and errors.
1.2.8 Manage referrals to ensure patients receive radiation dose as low as reasonable possible.
1.2.9 Supervising staff and patients in radiation work areas.
1.2.10 Provide support and reassurance to patience, taking into account their physical and psychological needs.
1.2.11 Documenting information with computers.
1.3 Core Competencies
Should demonstrate ability to provide high quality diagnostic imaging services, planning and giving treatment using x-rays and other radioactive resources.
1.4 Personal Specifications
Diploma in Diagnostic Radiography with Sonography must be registered by Tanganyika Medical Imaging and Radiology Council. A combination of relevant certified academic certificates. He/she must possess computer skills and should have at least 2 years working experience.
MODE OF APPLICATION
Candidates meeting the requisite qualifications should submit their written applications and detailed CV to the address below. describing how they see themselves qualifying for this position. They should also send certified copies of academic certificates, three references. daytime telephone numbers and e-mail addresses. The closing deadline for all applications is 16 June, 2017. Any application letter after the deadline will not be considered.
Only shortlisted candidates will be contacted
Human Resources Executive Officer, 
P. 0. Box 93, 
Moshi, Kilimanjaro
Tel: +255272754389, FAX:+255272754391
E-mail:'tpc@tpc.co.tz

Saturday

Spika ana mamlaka kisheria ya kuomba vyombo vya dola kumsaidia kumkamata mtu – Mdee

Spika ana mamlaka kisheria ya kuomba vyombo vya dola kumsaidia kumkamata mtu – Mdee

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee amesema Spika ana mamlaka ya kisheria ya kuomba vyombo vingine vya dola kumsaidia kumkamata mtu huku akisema kuwa ameamua kuwahi Dodoma kuepuka kukomolewa na Spika Ndugai aliyeagiza afike mbele ya Kamati ya Maadili jana asubuhi na kuagiza polisi wamsake popote alipo, ikiwezekana apelekwe akiwa amefungwa pingu.
Mdee, ambaye alikuwa Dar es Salaam wakati amri hiyo ikitolewa juzi saa 5:00 asubuhi, aliwasili Dodoma jana, lakini suala lake litajadiliwa leo. “Spika ana mamlaka ya kisheria ya kuomba vyombo vingine vya dola kumsaidia kumkamata mtu,” alisema Mdee alipoongea na gazeti la Mwananchi.
“Kwa sababu hiyo, ana uwezo wa kutumia mamlaka hayo kumkomoa mtu. Ndiyo maana nikaja mwenyewe Dodoma. Niliacha majukumu mazito niliyokuwa nayo ili lengo lake la kunikomesha lisifanikiwe,” aliongeza. Spika Ndugai, aliyezungumza kwa ukali, alisema anajua kuwa Mdee alikuwa nje ya Dodoma, lakini akataka awe amefika mbele ya kamati hiyo jana muda sawa na ule aliokuwa akitoa maagizo hayo juzi.
Mdee anatuhumiwa kutoa lugha mbaya kwa Spika, Rais na wabunge wakati wa mjadala uliokuwa mkali wa nafasi za wagombea wa Chadema na CUF katika Bunge la Afrika Mashariki.
Mdee pamoja na Kiongozi wa Kambi Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kufika watahojiwa na kamati hiyo leo.

Monday

Taarifa rasmi kutoka Clouds Media kuhusu video inayosambaa

Taarifa rasmi kutoka Clouds Media kuhusu video inayosambaa

Kufuatia kusambaa kwa video mitandaoni ikiaminika ni mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akiingia Clouds Media akiwa na askari, Uongozi wa Clouds Media Group umetoa taarifa rasmi leo March 19 2017.
Taarifa imesema…>>>’Kumekuwa na habari mbalimbali kuhusu Clouds Media Group na viongozi mbalimbali akiwemo Askofu Josephat Gwajima na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda. Kiini cha habari zote hizo ni uwepo wa taarifa zinazomhusu mwanamke anayedai kuzaa na Askofu Gwajima
Ni kweli habari ya uwepo wa mama huyo ilitufikia kupitia kipindi chetu cha De Weekend Chat Show (SHILAWADU) lakini baada ya uchunguzi wa kina tuligundua kwamba habari haina mashiko, inakosa vigezo vya habari inayofaa kuonyeshwa na hivyo tulisimama katika kanuni za taaluma yetu na kuzuia kabisa kuonyeshwa kwa taarifa hiyo
Kizuizi hicho kilifuatiwa na matukio mbalimbali ikiwemo mijadala inayosambaa juu ya Mkuu wa mkoa Paul Makonda kuvamia ofisizetu. Jambo hilo limezua hofu na taharuki kubwa kwa wadau wote pamoja na kusababisha mashaka miongoni mwa wafanyakazi na viongozi wa Clouds Media Group
Pamoja na yote jambo hili lipo katika uchunguzi wa kina unaofanywa na sisi Clouds Media Group kwa kushirikiana na mamlaka zote husika, tunaomba wapenzi, wadau na Watanzania wote wawe na subira wakati tunajiandaa kutoa tamko rasmi kuhusu yaliyotokea
.
Ifaham Gharama ya kuilinda familia ya Trump kwa siku

Ifaham Gharama ya kuilinda familia ya Trump kwa siku

Familia ya Rais wa Marekani, Donald Trump ina ulinzi mkali. Ulinzi huo unadaiwa kugharimu kiasi kikubwa cha fedha.
Wakati ambapo Trump alihamia kwenye ikulu ya White House iliyopo jijini Washington DC, mke wake Melanie, na mwanae wa mwisho, Barron bado wanaishi New York.
Muda mfupi baada ya uchaguzi, ripoti ya CNN Money ilionesha kuwa kuilinda familia ya Trump mjini New York hugharimu dola milioni 1 kwa siku.
Kama wakiamua kuungana na Trump White House, gharama hiyo itapungua kwa kiasi kikubwa.
Hilo si jambo pekee linalozungumzwa kwa sasa. Tangu mwaka uanze, Trump ameenda mapumzikoni mara nne huko Mar-a-Lago Florida. Kwa mujibu wa wachambuzi wa gazeti la Politico, safari hiyo hugharimu dola milioni 3 kila akienda.

Friday

Rais Magufuli mbioni kuhamia Dodoma

Rais Magufuli mbioni kuhamia Dodoma

Rais wa Jamhuri wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ametembelea uwanja wa Chamwino mkoani Dodoma na kuwahakikishia wananchi kuwa atahamia Dodoma hivi karibuni kama alivyoahidi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa pamoja na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo nchini (TBA) Elius Mwakalinga kuhusu kazi za ufyatuaji wa Matofali yatakayotumika katika ujenzi wa Ikulu Chamwino mkoani Dodoma
Hii ni taarifa yake:

Agizo la Mwakyembe ‘huna cheti cha kuzaliwa hakuna kufunga ndoa’ lafutwa na Rais Magufuli

Agizo la Mwakyembe ‘huna cheti cha kuzaliwa hakuna kufunga ndoa’ lafutwa na Rais Magufuli

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amelifuta agizo lililotolewa jana tarehe 16 Machi, 2017 na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe linalotoa sharti la kuwa na cheti cha kuzaliwa kwa watu wote watakaofunga ndoa kuanzia tarehe 01 Mei, 2017.
Rais Magufuli amefuta agizo hilo leo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari muda mfupi kabla ya kuondoka katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma na kurejea Jijini Dar es Salaam.
Dkt. Magufuli amesema Serikali haiwezi kuruhusu sharti hilo kutumika kwa kuwa litawanyima haki ya kuoa na kuolewa Watanzania wengi ambao hawana vyeti vya kuzaliwa, huku utaratibu wa kupata vyeti hivyo ukiwa bado unakabiliwa na changamoto nyingi kwa wanaohitaji.
Amesema mpaka sasa idadi ya Watanzania walio na vyeti vya kuzaliwa ni chini ya asilimia 20 huku wengi wao wakiwa ni wananchi waishio vijijini ambako ni vigumu kupata vyeti hivyo, na wengine wakiwa ni waliozaliwa kabla ya kuanza kutolewa kwa vyeti vya kuzaliwa nchini mwaka 1961.
“Kwa hiyo ndugu zangu Watanzania msiwe na wasiwasi wowote, endeleeni na utaratibu wenu wa kuoa na kuolewa kama kawaida na kama kuna kifungu chochote cha sheria kinachomlazimisha mtu awe na cheti cha kuzaliwa ndipo aoe ama aolewe nitamuelekeza Waziri wa Katiba na Sheria Harrison Mwakyembe apeleke Bungeni kikarekebishwe”-Rais Magufuli.
Rais Magufuli ametoa wito kwa wanasheria kuziangalia vizuri sheria zinazohusiana na kuzaliwa na kifo na kuoa na kuolewa ili zisilete mkanganyiko kwa wananchi. Hata hivyo Mhe. Rais Magufuli ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kupata vyeti vyao vya kuzaliwa kama kawaida na amewataka viongozi wote kuwahamasisha wananchi kuwa na vyeti hivyo.

Sunday

Jeshi la polisi Dar lakusanya milioni 840 kwa faini ya makosa mbalimbali ya barabarani

Jeshi la polisi Dar lakusanya milioni 840 kwa faini ya makosa mbalimbali ya barabarani

Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam limefanikiwa kukusanya jumla ya shilingi milioni 840 za faini ya makosa mbalimbali ya barabarani kwa kipindi cha wiki moja ya oparesheni iliyofanywa na jeshi hilo.

Akiongea na waandishi wa habari Ijumaa hii, Kamishna wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema kiwango cha mapato hayo ni kidogo na inaashiria kupungua kwa makosa yanayofanywa na madereva.
“Kwa upande wa barabarani tunakwenda vizuri kati ya tarehe 1 mwezi 3 mwaka 2017 mpaka tarehe 9 mwezi wa 3 mwaka 2017 takribani siku hizo 8 tumeweza kukusanya jumla ya shilingi milioni 840 kwahiyo niseme tu kwamba mapato yanapungua hii tu ni kwasababu watu wameanza kutii tu sheria ya usalama barabarani,” Alisema Kamanda Sirro.

Thursday

Kukamatwa kwa pombe za ‘viroba’ zasababisha mfanyabiashara ajiue

Kukamatwa kwa pombe za ‘viroba’ zasababisha mfanyabiashara ajiue

Oparesheni ya wafanyabiashara wa viroba inayoendelea nchini, imesababisha Mfanyabiashara mmoja ajiue kwa kujipiga risasi kichwani.
Mfanyabiashara huyo ni mmiliki wa kampuni ya Mselia Enterprises na duka la bia za jumla, baa na nyumba za kulala wageni mjini Dodoma. Alijipiga risasi kwenye shavu la kushoto juzi, Jumanne akiwa shambani kwake Veyula, nje kidogo ya mji wa Dodoma.
Daktari wa zamu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Carolyn Damian alisema alimpokea Mselia hospitalini hapo akiwa mahututi saa 7 usiku, na kumweka katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU) na robo saa baadaye alifariki.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Lazaro Mambosasa alithibitisha kupewa taarifa na mtu kuhusu kusikika kwa mlio wa risasi saa 3 usiku na baadaye saa 5 aliwatuma askari na kwenda kuchunguza na ndipo walipomwona mfanyabiashara huyo, amejipiga risasi na alikufa kutokana na kutokwa na damu nyingi.
Mambosasa alisema baada ya kupewa taarifa, askari walifuatilia eneo ambalo risasi zilisikika katika shamba la mfanyabiashara huyo eneo la Veyula na walipofika, waliokota maganda matano ya risasi alizotumia kujiua.
Mfanyakazi wa mfanyabiashara huyo, Leslie Msigwa alisema ni kweli polisi walikwenda mara mbili dukani kwake Barabara ya 11, karibu na Ofisi za TFDA, na mara ya mwisho waliondoka naye akiwa kwenye gari lake prado likiendeshwa na mteja wao, Mazengo hadi waliposikia kwamba amejiua shambani kwake, Veyula Dodoma.
Msigwa alisema ni kweli kwenye stoo yake, kulikuwa na katoni 1,269 za viroba pamoja na vinywaji vingine, ambavyo huwa wanasambaza katika baa na maduka mbalimbali.
Msigwa alisema Ijumaa iliyopita, polisi walifika dukani kwake wakiwa kwenye magari mawili wakiwa na silaha, wakaingia kukagua ndani na wakaondoka na wao, wakaenda benki kuweka fedha na kulipia mzigo iliyoagizwa.
Kampeni hiyo ya kuzia pombe aina hiyo nchini, inayosimamiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira ilianza Machi mosi mwaka huu, baada ya Serikali kutoa taarifa ya mwisho wa biashara hiyo tangu Mei, mwaka jana.
Mei mwaka jana, Serikali ilibainisha kuwa kuanzia kipindi hicho hadi Januari mosi mwaka huu, ungekuwa mwisho wa kuzalisha na biashara ya pombe kali inayohifadhiwa katika vifungashio hivyo (viroba).

Saturday

TID kumshtaki Steve Nyerere, ni baada ya kutuhumiwa kupokea milioni 2 za RC Makonda

TID kumshtaki Steve Nyerere, ni baada ya kutuhumiwa kupokea milioni 2 za RC Makonda

Msanii mkongwe wa muziki Khalid Mohamed ‘TID’ ameahidi kuwachukulia hatua watu wanaosambaza taarifa kuwa alipewa pesa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kama kivuli katika sekeseke la kutaja majina ya wanaohusika na dawa za kulevya.
Muimbaji huyo alisema yeye alikuwa ni muathirika wa dawa za kulevya na serikali ilimkamata kwa kosa la kutumia lakini ikaamua kumsaidia kwa kumfanya aachane na dawa hizo pamoja na kumpa nafasi ya kuelimisha vijana wenzake ambao bado wapo katika janga hilo.
“Watu wana ushahidi gani kama mimi Mh. Makonda kanipa mimi pesa au wanazungumza tu? mimi nataka huyo sijui Steve nani nani…..aseme kwamba aliniona nikipatiwa hizo pesa bila hivyo mimi nitamshtaki, unaituhumu serikali, bila ushahidi, hili ni kosa ambalo naweza nikampeleka mtu mahakamani,” TID alikiambia kipindi cha Selekt cha EATV.
Msanii anayedaiwa kutoa kauli hiyo ya TID kupewa pesa ni Steve Nyerere, kupitia sauti za simu zilizosambazwa tangu juzi, zikionesha mtu anayedhaniwa kuwa ni Steve Nyerere akiongea na mtu anayedhaniwa kuwa ni Mama wa msanii Wema Sepetu.

Thursday

Rufaa ya Trump kurudisha marufuku ya waislamu kuingia US yapigwa chini, sasa ruksa

Rufaa ya Trump kurudisha marufuku ya waislamu kuingia US yapigwa chini, sasa ruksa

Mahakama ya rufaa nchini Marekani imelikataa jaribio la Rais wa nchi hiyo, Donald Trump kurejesha amri yake ya kuzuia wageni kutoka nchi saba za kiislamu kuingia nchini humo.
Mahakama hiyo imesema haitoweza kuzuia agizo lilitolewa na mahakama ya chini yake. Trump aliujibu uamuzi huo kwa hasira kwenye Twitter akidai usalama wa nchi upo matatani.
Majaji watatu kwenye mahakama hiyo wamekubaliana pamoja wakidai kuwa serikali haijatoa uthibitisho wa uwepo wa tishio la kigaidi kuhalalisha marufuku hiyo. Uamuzi huo una maanisha kuwa watu kutoka Iran, Iraq, Libya, Somalia, Sudan, Syria na Yemen walio na visa wanaweza kuingia Marekani.
Na wakimbizi kutoka duniani kote waliokuwa wameathirika na marufuku hiyo nao hawatazuiwa tena.
Kesi hiyo itaendelea kusikilizwa kwenye mahakama kuu.
Rais Magufuli amsimamisha kazi Kaimu Katibu wa Tume ya Mipango

Rais Magufuli amsimamisha kazi Kaimu Katibu wa Tume ya Mipango

Rais John Magufuli amemsimamisha kazi Kaimu Katibu wa Tume ya Mipango (Wizara ya Fedha), Florence Mwanri aliyeidhinisha kuanza kwa awamu ya pili ya ujenzi wa jengo jipya la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) (Terminal 3) kabla ya kumalizika kwa awamu ya kwanza ili kupisha uchunguzi.
Rais Magufuli alichukua uamuzi huo baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika mradi wa ujenzi wa jengo jipya na kuagiza shughuli za ujenzi wa uwanja huo ziendelee kuanzia leo.
Taarifa iliyotolewa Jumanne hii na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa ilieleza kuwa Rais Magufuli alisikitishwa na namna mradi huo unavyotekelezwa, ikiwamo Serikali kukubali gharama kubwa za mradi ambazo ni Shilingi 560 bilioni kiwango ambacho ni kikubwa ikilinganishwa na jengo linalojengwa.
“Hivi kulikuwa na sababu gani za ninyi wataalamu wa serikali kukubali gharama kubwa namna hii, hivi hili jengo linafanana na Shilingi 560 bilioni? alihoji. Halafu mlikuwa na haraka gani kuidhinisha kuanza awamu ya pili ya ujenzi kabla ya kumaliza awamu ya kwanza?” aliendelea kuhoji Rais Magufuli.
Katika ziara aliyoifanya jana ilielezwa kuwa mkandarasi anayejenga uwanja huo, kampuni ya BAM International alitangaza kusitisha ujenzi kuanzia jana kutokana na kutolipwa madai yake. Hata hivyo, Rais Magufuli ameahidi kulipa fedha hizo haraka.
Aidha Rais Magufuli ameviagiza vyombo vinavyohusika kufanya uchunguzi katika mradi huo.
Tundu Lissu apandishwa kizimbani

Tundu Lissu apandishwa kizimbani

Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam akikabiliwa na mashtaka manne ya uchochezi.
Lissu amepandishwa kizimbani saa 6:25 na kusomewa mashtaka hayo na Wakili wa Serikali Kishenyi Mutalemwa. Mutalemwa amesema upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea lakini akawasilisha maombi ya kupinga dhamana ya mshtakiwa.
Katika maombi hayo amesema mshtakiwa Lissu anakabiliwa na kesi nyingine tatu mahakamani hapo na kwamba ingawa yuko nje kwa dhamana lakini amekuwa na mwenendo unaohatarisha amani si tu kwa wanajamii, bali hata kwake mwenyewe kwa kuendelea kutoa maneno ya uchochezi.
Hata hivyo maombi hayo yalipingwa na Wakili wa Lissu Peter Kibatala akisema kuwa mashtaka yake yanadhaminika. Amesema kiapo cha kupinga dhamana kilichotolewa na mkuu wa upelelezi wilaya ya Ilala, ASP Denis Mjumba kina dosari za kisheria kwani hakikidhi masharti ya viapo.
Mabishano bado yanaendelea, Wakili Kibatala bado anatoa hoja kabla ya Hakimu Huruma Shaidi kutoa uamuzi.

Monday

Vita ya dawa za kulevya: 12 kati ya 112 kupandishwa kortini akiwemo Wema, TID na wengine

Vita ya dawa za kulevya: 12 kati ya 112 kupandishwa kortini akiwemo Wema, TID na wengine

Sakata la Madawa ya kulevya limeendelea kugonga vichwa vya habari wiki hii ambapo Jumatatu hii Jeshi la polisi limedai toka lianze operesheni hiyo tayari limewakamata watuhumiwa 112 na kati ya hao 12 watapandishwa mahakamani Jumatatu hii kwajili ya kiapo cha kutorudia matumizi ya Madawa ya kulevya baada ya kukiri kutumia.


Kati ya watu hao 12 ni pamoja na Wema Sepetu, Romy Jones, Petit Man, TID pamoja na wengine.
Aidha Wema Sepetu baada ya kiapo hicho atarudishwa polisi kwajili ya kuandaliwa shtaka jipya linalomkabili la kukutwa na msokoto wa bangi nyumbani kwake.
Akiongea na waandishi wa habari Jumatatu hii, Kamanda wa Polisi wa Kanda maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema watuhumiwa wengi waliohojiwa walikiri kutumia Madawa ya kulevya na kati ya hao walieleza watu ambao wanawauzia.
“Tumewakamata watuhumiwa jumla 112 na tumekamata kete 299 zinazodhaniwa ni za Madawa ya kulevya na kwa kawaida haya Madawa Mkemia Mkuu wa serikali yeye ndiye atakayetuambia ni Madawa ya aina gani,” alisema Kamanda.
Aliongeza, “Katika watuhumiwa 112, kuna watuhumiwa 12 tunawapeleka leo mahakamani, tunawapeleka mahakamani kwa sababu sheria ya mwenendo wa mashtaka iko wazi kifungu cha 73 na 74, huwa tunaweza kuomba kwa mweshimiwa hakimu kuwaombea watuhumiwa kwa kiapo, kwamba hawa watuhumiwa tunataka wabadilishe tabia zao. Tunawapeleka mahakamani ili wache chini ya uangalizi wa jeshi la polisi na mahakama kwa muda wa miaka 2 wasifanye makosa tena,”
“Kwa sababu tulichokibaini kwa wote tuliowakamata wengine wanakiri na wamekwenda kuonyesha hayo Madawa ya kulevya. Kwa hiyo kusudio la kwanza wawe chini ya uangalizi wetu, na kusudio la pili la kiapo chetu waache hiyo tabia ili wabadilike wawe raia wema, lakini la tatu tumeomba wale wanakuja kuripoti kituoni angalau mara mbili kwa mwezi na lengo letu ni kuona hawa ndugu zetu ambao walikiwa wanavuta madawa ya kulevya wamecha kabisa,”
Fahamu unywaji pombe salama unaoweza kuimarisha afya yako

Fahamu unywaji pombe salama unaoweza kuimarisha afya yako

Kipimo salama na sahihi kwa afya bora cha unywaji wa pombe kinabadilika kutokana na umri. Ongea na mfamasia wako kujua ni kiasi gani ni mahususi kwa afya yako.

Hakuna shaka umewahi kusikia kwamba unywaji wa wastani wa bia moja hadi mbili kwa siku kwa mwanamme husaidia kuimarisha afya yako na kukuepusha na magonjwa ya moyo. Lakini hata kama pombe ni rafiki au adui wa afya yako inategemea na vitu viwili; Hali yako ya afya ya sasa na ni kiasi gani cha pombe unachotumia. Ushauri kwa mtu mmoja mmoja ni mzuri zaidi.
Kwa baadhi ya watu inategemea na aina ya dawa wanazotumia na mambo mengine, utumiaji wa pombe hata kwa wastani inaweza kuwa ni hatari kwa afya yako.
Unywaji wa wastani kwa afya yako. Tafiti mbalimbali zimeonyesha kuwa watumiaji wa wastani wa pombe wanapunguza hatari ya kupata shinikizo la moyo na kiharusi, kisukari na huimalisha mifupa kwa wazee zaidi ya watu wanaokunywa kidogo sana au wasiokunywa kabisa.
Ninapozungumzia wastani namaanisha vinywaji viwili kwa siku kwa mwanaume na kimoja kwa wanawake. Watu wengine huepukana na unywaji wa pombe kwa sababu ni wagonjwa au sababu anatumia dawa zinazokinzana na pombe. Unywaji wa pombe kupita kiasi ni hatari kwa afya yako kwani zinaweza kukusababishia magonjwa ya moyo,kiharusi na aina Fulani za kansa ingawaje watumiaji wengi wa pombe huwa wanavuta sigara pia.
Baadhi ya matatizo yanayoweza kukufanya usinywe pombe;
• Kama unatumia dawa zinazosinyaza damu (the blood-thinning medication) warfarin (Coumadin),pombe husababisha tatizo la kutokwa na damu.
• Kama unafanya jitihada za kupunguza shinikizo la damu, hata kama utakunywa bia mbili kwa siku inaweza kupandisha BP yako.
• Unywaji wa wastani husaidia watu wanaohiyaji kupunguza uzito.
Tafiti nyingi zimeonyesha watu wanaokunywa bia mbili mpaka sita kwa wiki wanapunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo (cardiovascular disease) zaidi ya watu wanaokunywa zaidi. Watu wenye umri wa zaidi ya miaka 65 wanaume kwa wanawake inabidi angalau wanywe bia moja kwa siku. Bia mbili kwa siku zinaweza zisiimalishe afya yako licha yakuwa sihatari kwa afya yako.
Ni vigumu sana kusema kuwa kiasi fulani ndo sahihi kwasababu tafiti nyingi za kisayansi zinaonesha utofauti kutokana na utofauti uliopo baina ya mtu na mtu na jamii inayowazunguka.
Kama haunywi pombe usijaribu kuanza kunywa kabisa kwa matarajio ya kuimarisha afya yako. Ni vema ukaanza mazoezi, ukila vyakula vya kujenga mwili na matunda na usijaribu kuvuta sigara kabisa. Ukizingatia vitu hivi utaimalisha afya yako kwa kiasi kikubwa.
“Kwa watu ambao hawanywi pombe kabisa, ushauri wangu wasijaribu kunywa kabisa, kwani kuna njia nyingi za kukufanya kuwa na afya bora kuliko kuanza kutumia pombe na kuanza kukubwa na athari nyingi za kiafya zinazosababishwa na matumizi ya kupindukia ya pombe.”
Kiasi sahihi ya pombe kinachoshauriwa kiafya ni kama kinavyoonekana kwenye jedwali lifuatalo
Vinywaji vingine vya pombe vina nguvu kuliko vingine. Kwahiyo ni vizuri kuangalia ni kiasi gani kinachokufaa kiafya, kwa mfano cocktile zingine unaweza kuona zipo kwenye glasi ndogo lakini kumbe ina nguvu zaidi ya bia tatu mpaka nne.
Your Health, Our Concern
Polisi wamzuia Askofu Mokiwa kushiriki ibada

Polisi wamzuia Askofu Mokiwa kushiriki ibada

Polisi wameingilia kati mvutano ndani ya Kanisa la Anglikana baada ya kumzuia Askofu wa Dayosisi ya Dar es Salaam, Dkt. Valentino Mokiwa kushiriki ibada ya kumsimika Askofu mpya wa Dayosisi ya Lweru.
Askofu Mokiwa amekuwa katika mvutano na Askofu Mkuu wa Anglikana Tanzania, Dkt. Jacob Chimeledya tangu alipotangaza kumvua uongozi wa Dayosisi ya Dar es Salaam, akidai mkuu huyo hakufuata utaratibu na kwamba hana mamlaka ya kuchukua uamuzi huo.
Aidha Askofu Mokiwa aliwasili makao makuu ya Dayosisi ya Lweru mjini Muleba mkoani Kagera na alitarajiwa kuungana na maaskofu wengine kumsimika Godfrey Mbelwa kuwa askofu mpya wa dayosisi hiyo.
Lakini taarifa zilizopatikana zimesema Askofu Mokiwa alichukuliwa na polisi na kuhojiwa katika kituo cha Muleba, kutokana na kuhofu kuwa kuwapo kwake kungeweza kusababisha vurugu katika ibada iliyokuwa iongozwe na Dkt. Chimeledya kutokana na mvutano uliopo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera Augustino Ollomi,amesema kuwa jeshi hilo halikumkamata Askofu Mokiwa na kumhoji, badala yake amesema walichukua hatua haraka baada ya kupata taarifa za kiintelijensia kuhusu masuala ya usalama. “Ni wajibu wetu kufuatilia, tulimuonya kuhusu suala la kuhudhuria ibada kwa sababu kulikuwa na viashiria vya uvunjifu wa amani lakini ilikuwa ni hiari yake kutohudhuria, huo utakuwa ni uamuzi wake,” amesema Ollomi.

Thursday