Showing posts with label UJASILIAMALI. Show all posts
Showing posts with label UJASILIAMALI. Show all posts

Monday

Kulala chali kwa mjazito ni hatari kwa mtoto

Kulala chali kwa mjazito ni hatari kwa mtoto

Wanawake wajawazito wanaopenda kulala chali  wapo kwenye hatari  ya kuzaa mtoto mfu(stillbirth),kulingana na wanasayansi.

Katika utafiti  uliofanyika nchini Ghana, wanawake wajawazito ambao walipenda kulala chali wakati wa ujauzito  walikuwa  kwenye hatari mara tano zaidi ya kuzaa watoto wenye uzito mdogo na  kwa wanawake wengine walizaa watoto wafu.

Utafiti huu ulifanyika nchini Ghana kutokana na kuwa kati ya watoto 1000 wanaozaliwa 20 hadi 50 kati yao huwa ni watoto wafu.Hata hivyo, utafiti mpya uliofanyika nchini New Zealand pia umehusisha kulala chali kwa mwanamke mjamzito na idadi kubwa ya  watoto wafu wanaozaliwa  katika nchi zenye raia wenye kipato kikubwa.

Mkuu wa utafiti huu,Louise O'Brien  kutoka chuo kikuu cha Michigan, nchini Marekani amesema kama kutokulala chali wakati wa ujauzito hupunguza uwezekano wa kuzaa mtoto mfu basi ni vizuri kuhamasisha kina mama wajawazito kutolala chali kwani hii ni njia rahisi na isiyokuwa na gharama yoyote ile.

Tabia hii ya kulala chali wakati wa ujauzito inaweza kuepukika kwa kuwashauri  kina mama wajawazito madhara yanayopatikana kwa kulala chali.

Matokeo ya utafiti huu yanaonyesha ya kwamba zaidi ya robo ya idadi ya watoto wanaozaliwa wafu inaweza kuepukika kwa kubadilisha staili ya kulala tu kwa wanawake wajawazito.

Siku zote madaktari wanashauri kina mama wajawazito kulala ubavu mmoja hasa upande wa kushoto ili kuepuka kuzaa mtoto mfu au mtoto mwenye uzito mdogo kwa sababu mwanamke mjazito anapolalia ubavu wake wa kushoto huongeza mzunguko wa damu kwa kiumbe kilichomo ndani yake.

Utafiti huu uliofanyika nchini Ghana unaunga mkono utafiti uliofanyika hivi karibuni nchini Australia unaojulikana kama Sydney Stillbirth Study ambao ulisema ya kwamba wanawake wanaolala chali wakati wa ujauzito wako kwenye hatari ya mara sita zaidi ya kuzaa watoto wafu.Utafiti huu wa Australia ulifanyika kwa miaka mitano na ulihusisha wanawake wajawazito 295 kutoka katika hospitali nane nchini Australia.

Naye mtafiti mkuu katika utafiti huu Dr. Adrienne Gordon, kutoka Sydney's Royal Prince Alfred Hospital amesema “Tafiti za awali zilionyesha ya kwamba wanawake wanaolala chali wakati wa ujauzito, hupunguza mzunguko wa damu unaotakiwa kwenda kwa mtoto.Lakini  pia ni vizuri kwa wanawake ambao ni wajawazito  kutotaharuki kama wakati mwingine watalala chali.’’Kutokana na idadi ndogo ya wanawake wajawazito waliohusishwa kwenye utafiti huu sisi wana Tanzmed tunachelea kusema ya kwamba ni vigumu kusema utafiti huu umetoa mapendekezo sahihi ya  namna ya kulala kwa wanawake wajawazito.

Pia kutokana na kutoangalia muda ambao wanawake hao walilala wakiwa chali (mfano kama walilala masaa 4,6 au 8 kwa siku na kwa siku ngapi) na tofauti ya hatari kati ya wanawake wajawazito waliolala muda mfupi na mrefu, hivyo tunawaambia wanawake wajawazito kutohofu kama watalala chali lakini ni bora kuchukua tahadhari mapema.Tafiti hii inatoa changamoto kwa watafiti wetu wa afya kuangalia jinsi ya kufanya tafiti kama hizi katika mazingira ya kwetu.
Chakula cha mtu mwenye Vidonda vya Tumbo

Chakula cha mtu mwenye Vidonda vya Tumbo


Hapo kabla tulisoma kwa kirefu kuhusu vidonda vya tumbo kisha tukasoma kuhusu dawa mbadala ya vidonda vya tumbo na leo tunaendelea kuangalia chakula cha mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

Katika kutibu vidonda vya tumbo, mara nyingi ni lazima kupunguza uzalishaji wa asidi tumboni au mwilini kwa ujumla.

Matibabu ya vidonda vya tumbo hujumuisha lishe na kubadilisha mitindo ya maisha na kutumia dawa maalumu.

Ikiwa matatizo kama kuvuja damu au vitobo sehemu ya kidonda yatatokea, basi hapo upasuaji huwa ni muhimu.

Vidonda vya tumbo kwa ujumla hupona ndani ya wiki 4 mpaka 6 za matibabu.
Mtu mwenye vidonda vya tumbo ni mtu mwenye asidi nyingi mwilini kuliko alkalini, hivyo anatakiwa kupendelea zaidi kula matunda na mboga za majani. Anahitaji zaidi ukijani mwilini mwake. Pia apendelee kula ugali wa dona kuliko ugali wa sembe na inashauriwa pia kupunguza kula wali.

Kitu kingine mhimu kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo ni maji. Hakikisha unakunywa kila siku maji glasi 8 hadi 10.

MAZOEZI MAALUMU KWA ANAYESUMBULIWA NA MIGUU KUWAKA MOTO AU ASIDI KUZIDI MWILINI
Unalala chali, nyoosha mikono chini. Kisha nyanyua mguu mmoja juu unyooke, shusha chini mguu na unyanyuwe wa pili hivyo hivyo juu kisha chini. Endelea hivyo hivyo kwa mara kumi kumi kwa round 5. Zoezi lichukuwe dk 10

Nyanyuka na ujipigie saluti mwenyewe ukianzia mkono wa kulia mara 15 hamia mkono wa kushoto mara 15 tena kwa round 5

Kisha simama, chuchumaa simama, chuchumaa simama, hivyo hivyo mara 15 kwa round 5

Pia unasimama wima, nyoosha mikono yote juu na uishushe mabegani. Hivyo hivyo mikono juu mikono mabegani mara 15 kwa round 5

Fanya hivi mara 4 mpaka 5 kwa wiki.
Hapa chini nimekuwekea jedwali la jumla la vyakula na vinywaji vyenye asidi sana, asidi ya kati na alkalini sana, vile vya kuviepuka ni vile vyenye asidi sana, orodha itaendelea kuboreshwa;

Mayai na bidhaa za maziwa

  • Alkaline: mtindi
  • Neutral: mtindi mtupu (plain Yogurt ),
  • Acid: siagi, krimu, mayai, jibini ngumu (Hard Cheese), Ice Cream, jibini ya kiwandani (Processed Cheese), maziwa

Vyakula jamii ya maharage

  • Alkaline: Lima, njegere, Snap, String
  • Neutral: Soya
  • Acid: Black, Garbanzo, Kidney, dengu

Vyakula jamii ya karanga

  • Alkaline: lozi, Nazi freshi (fresh)
  • Neutral:
  • Acid: Brazil, korosho, Nazi kavu (dried coconut), Macadamia, karanga, Pecan, Pistachio, Walnut

Mboga za majani

  • Alkaline: asparaga (Asparagus), kiazisukari (Beets), brokoli (broccoli), kabeji, karoti, Koliflawa (aina ya kabichi – Cauliflower), figili (Celery), tango, mwani (Kelp), saladi (Lettuce), uyoga, vitunguu, kotimiri (Parsley), Bell Peppers, viazi ambavyo havijamenywa (with skin), boga (Squash), nyanya
  • Neutral: Horseradish, Rhubarb, Sauerkraut
  • Acid: Spinachi iliyopikwa, viazi ambavyo vimemenywa (no skin Potato), achali

Matunda

  • Alkaline: tufaa (Apple), parachichi, tende, mtini, zabibu, balungi, Kiwi, Limau, ndimu, embe, tikiti maji, chungwa, mpichi, Pears, Stroberi
  • Neutral:
  • Acid: Blueberry, Cranberry, plamu (Plum), plamu kavu (Prune)

Vinywaji

  • Alkaline: Maji ya limau, Chai ya tangawizi
  • Neutral: Maji
  • Acid: Chai ya rangi, Bia, kahawa, vinywaji vyenye kafeina, juisi za viwandani (processed), Liquor, Soda, Wine

Viongeza utamu

  • Alkaline: Asali mbichi (Raw Honey), sukari mbichi (Raw Sugar), Stevia
  • Neutral:
  • Acid: Viongeza utamu vyote vya kutengenezwa (Artificial Sweeteners)

Nyama

  • Alkaline:
  • Neutral:
  • Acid: Nyama ya ng’ombe, kuku, Samaki, mbuzi, batamzinga, nyama ya nguruwe, Sungura

Mafuta

  • Alkaline: mafuta ya mbegu za katani
  • Neutral: mafuta ya lozi, Canola, mafuta ya nazi, mafuta ya mahindi, Margarine, mafuta ya zeituni, Safflower, mafuta ya ufuta, mafuta ya Soya, mafuta ya alizeti
  • Acid:

Vitafunwa & nafaka

  • Alkaline: Amaranth, Millet, Quinoa
  • Neutral:
  • Acid: Barley, Buckwheat, Oats, mchele, Rye, Spelt, ngano, Pasta (vyakula jamii ya tambi), biskuti

Mbegu

  • Alkaline: Alfalfa (sprouted), chia (sprouted), Sesame (sprouted)
  • Neutral:
  • Acid: boga, alizeti, ngano

Sunday

Newz: Mambo Matano Yaliyo Iangusha Timu Ya Simba Yasome Hapa

Newz: Mambo Matano Yaliyo Iangusha Timu Ya Simba Yasome Hapa

  
  1. Eneo la kiungo la Simba

Safu ya kiungo ya Simba ilibadili mchezo wao wa pasi nyingi hasa baada ya Yanga kuanza mchezo kwa kasi wakitumia mipira mirefu kutoka kwa Kamusoko kwenda kwa Niyonzima na Ngoma kitu ambacho kilimfanya Tambwe awe huru zaidi na madhara ya Ngoma yalionekana kutokana na usumbufu wake akamsababishia kadi Nyekundu mlinzi Banda.

 

  1. Morali ya wachezaji baada ya Kadi  Nyekundu

Wachezaji wa simba walionekana  kutokukubaliana na kadi ya Banda hali ambayo iliwatoa mchezoni kwa muda akiwemo kiungo Mwinyi Kazimoto ambaye hakucheza kama alivyozoeleka kwenye Mechi za hivi karbuni na hali hii ilikuja baada ya kiungo Majavi kulazimika kurudi nyuma kucheza beki na Juuko..Kiungo cha Simba kilikatika na kutoa nafasi kwa Niyonzima kucheza pamoja na Kamusoko wakiwalisha vizuri washambuliaji wao.

 

  1. Kasi na Utulivu wa Donald Ngoma

Ngoma amechangia kwa kiasi kikubwa ushindi wa jana baada ya kuwa msumbufu na muda wote akikaa eneo la kumi na Nane ya Simba kitu ambacho kiliwanyima uhuru mabeki wa simba kuanziana pasi fupi na matokeo yake aliweza kukaa eneo zuri na akatumia makosa ya Kessy na kuandika bao la kwanza.

 

  1. Mabadiliko ya Kocha Mayanja 

Baada ya mapumziko Kocha wa simba aliamua kupumzisha Kazimoto ambaye alionekana kuumia na kucheza chini ya kiwango lakini hakupiga vizuri hesabu zake..kwangu mimi naona alitakiwa kuingiza beki atakaye cheza na Juuko kisha kumpandisha Majavi kwenye nafasi ya kiungo wa kati ili kusaidiana na Mkude lakini haikuwa ivyo aliona amwingize kiungo ambaye bado hakuwa na uzoefu wa pambano kubwa kama hilo na matokeo yake alipwaya na kumulazimu Ajib kurudi kusaidia viungo huku mbele wakimwacha Kiiza peke yake.

 

  1. Kuingia kwa Mwashuya na Simon Msuva 

Bao hili liliwatoa simba mchezoni na kuwafanya wacheze nyuma zaidi bila ya kuwa na mashambulizi ya uhakika.

Mechi ilikuwa nzuri kila upande umejaribu kuonesha nini ambacho wamevuna kwa walimu wao na hatimaye bahati ikaanguka kwa Yanga na kuibuka na pointi zote sita msimu huu.

CHANZO_mtembezi.com