Showing posts with label ENTERTAINMENT. Show all posts
Showing posts with label ENTERTAINMENT. Show all posts

Sunday

Newz: Mambo Matano Yaliyo Iangusha Timu Ya Simba Yasome Hapa

Newz: Mambo Matano Yaliyo Iangusha Timu Ya Simba Yasome Hapa

  
  1. Eneo la kiungo la Simba

Safu ya kiungo ya Simba ilibadili mchezo wao wa pasi nyingi hasa baada ya Yanga kuanza mchezo kwa kasi wakitumia mipira mirefu kutoka kwa Kamusoko kwenda kwa Niyonzima na Ngoma kitu ambacho kilimfanya Tambwe awe huru zaidi na madhara ya Ngoma yalionekana kutokana na usumbufu wake akamsababishia kadi Nyekundu mlinzi Banda.

 

  1. Morali ya wachezaji baada ya Kadi  Nyekundu

Wachezaji wa simba walionekana  kutokukubaliana na kadi ya Banda hali ambayo iliwatoa mchezoni kwa muda akiwemo kiungo Mwinyi Kazimoto ambaye hakucheza kama alivyozoeleka kwenye Mechi za hivi karbuni na hali hii ilikuja baada ya kiungo Majavi kulazimika kurudi nyuma kucheza beki na Juuko..Kiungo cha Simba kilikatika na kutoa nafasi kwa Niyonzima kucheza pamoja na Kamusoko wakiwalisha vizuri washambuliaji wao.

 

  1. Kasi na Utulivu wa Donald Ngoma

Ngoma amechangia kwa kiasi kikubwa ushindi wa jana baada ya kuwa msumbufu na muda wote akikaa eneo la kumi na Nane ya Simba kitu ambacho kiliwanyima uhuru mabeki wa simba kuanziana pasi fupi na matokeo yake aliweza kukaa eneo zuri na akatumia makosa ya Kessy na kuandika bao la kwanza.

 

  1. Mabadiliko ya Kocha Mayanja 

Baada ya mapumziko Kocha wa simba aliamua kupumzisha Kazimoto ambaye alionekana kuumia na kucheza chini ya kiwango lakini hakupiga vizuri hesabu zake..kwangu mimi naona alitakiwa kuingiza beki atakaye cheza na Juuko kisha kumpandisha Majavi kwenye nafasi ya kiungo wa kati ili kusaidiana na Mkude lakini haikuwa ivyo aliona amwingize kiungo ambaye bado hakuwa na uzoefu wa pambano kubwa kama hilo na matokeo yake alipwaya na kumulazimu Ajib kurudi kusaidia viungo huku mbele wakimwacha Kiiza peke yake.

 

  1. Kuingia kwa Mwashuya na Simon Msuva 

Bao hili liliwatoa simba mchezoni na kuwafanya wacheze nyuma zaidi bila ya kuwa na mashambulizi ya uhakika.

Mechi ilikuwa nzuri kila upande umejaribu kuonesha nini ambacho wamevuna kwa walimu wao na hatimaye bahati ikaanguka kwa Yanga na kuibuka na pointi zote sita msimu huu.

CHANZO_mtembezi.com

Sunday

Aliyekua Mshindi Wa Airtel Trace Music Stars 2015 Mayunga Mbioni Kukamilisha Kolabo Yake Na Akon...

Aliyekua Mshindi Wa Airtel Trace Music Stars 2015 Mayunga Mbioni Kukamilisha Kolabo Yake Na Akon...


Mwimbaji wa Tanzania, Mayunga Nalimi ambaye ni mshindi wa Airtel Trace Music Stars 2015 anatarajia kuondoka nchini Jumatatu (Nov. 16), kuelekea New York, Marekani kwajili ya kurekodi wimbo na mwimbaji mwenye asili ya Senegal, Akon.

Kupitia kipindi cha XXL cha Clouds Fm, Mayunga ametaja mambo matatu anayokwenda kufanya Marekani.

“…naenda kupata hiyo mentorship, kufanya wimbo, na vilevile kushoot video ya wimbo ambao nitaufanya” alisema Mayunga.
Ameongeza kuwa wimbo anaoenda kurekodi utaandikwa na Akon mwenyewe.

“Hiyo ni project ya Akon kwasababu dili ni kwamba atakuwa anakuandikia wimbo yeye…”

Kutokana na ushindi huo, Mayunga alishinda mkataba wa kurekodi muziki na label ya Universal Music Group wenye thamani ya $500,000 ambayo ni takribani shilingi bilioni 1 pamoja na kurekodi wimbo na Akon.

Mwezi July, Mayunga alienda Afrika Kusini kushoot video yake ya kwanza ‘Nice Couple’ ambayo ilitambulishwa exclusive na Trace Urban July 31.

Tuesday

Diamond Platnumz -"Itakuwa History na kumbukumbu hadi ntakapozikwa"Soma Hapa...

Diamond Platnumz -"Itakuwa History na kumbukumbu hadi ntakapozikwa"Soma Hapa...

Diamond Platnumz amepost kwenye Account yake ya mtandao wa Instagram na kusema haya;

Diamond Platnumz
Nasibu Abdul Jumma (born 2 October 1989), popularly known by his stage name Diamond Platnumz (or simply Diamond), is a Bongo Flava recording artist and dancer from Tanzania. He is best known for his hit song “Number One”. Diamond has won numerous awards at Channel O and the Prestigious HiPipo Music Awards. He performed at the Big Brother Africa 7 eviction show in May 2012 and also toured Europe,america and asia.[2] Diamond is considered influential among his fans especially Maria J, and is said to be the most loved and decorated Tanzanian artist at the moment.[3] He is believed to be the highest selling Tanzanian artist of ringtones by mobile phone companies curently, as well as being among the artists earning the highest income in the African Great Lakes region’s music industry.[3] Also Diamond Platnumz holds a record of the highest paid artist in East Africa per One Show Diamond platnumz was paid 100 million Tsh in one show known as Tigo Kiboko Yao Concert his biggest steps curently was winning the MTV ema’s best worldwide act.

Thursday

Mgalilaya Kuachia Video Zake Mbili Hivi Karibuni...

Mgalilaya Kuachia Video Zake Mbili Hivi Karibuni...

Akiongea na SYLI CLASSIC BLOG mwanamuziki wa kizazi kipya Sebastian Mluta ali maarufu Kama Mgalilaya amesema yuko mbioni kuziachia video zake mbili kwa wakati tofauti tofauti kabla ya mwaka kuisha,Moja ya video ni ya wimbo uliofanya vizuri sana unaokwenda kwa jina la 'NIMO' pamoja na video nyingine ya wimbo wake mpya amemshirikisha Mesen Selekta unaitwa 'FINAL' Mgalilaya ameahidi kutowaangusha mashabiki wake hivo wakae mkao wa kula ili awape kitu roho inapenda,Usiache kutembelea blog yetu ili usizikose kazi zote za Mgalilaya zitakazokuwa zinaingia katika soko la muziki,Asante

Wednesday

Ali kiba ajibu kwa nini huwa haendagi kwenye tuzo....

Ali kiba ajibu kwa nini huwa haendagi kwenye tuzo....


Ali Kiba ambaye ni staa wa bongofleva alipita kwenye studio za Mtangazaji Millard Ayo na kuelezea mipango yake anapokwenda Marekani November 4 2015, kwanini huwa haudhurii matukio ya utolewaji wa tuzo mbalimbali anazowania, single mpya na Christian Bella na mengine.
Kwenye hii video hapa chini Ali Kiba amezungumzia pia single yao mpya na Christian Bella ‘nagharamia‘ ambayo wanaidrop Ijumaa hii

Monday

Chege Kufanya Kolabo na Mafikizolo.........

Chege Kufanya Kolabo na Mafikizolo.........




  leo Novemba 2, 2015  ni kwamba Chege Chigunda ana mpango wa kufanya kazi na Mafikizolo wa South Africa ambao ni mastaa wa hit single ya ‘khona’ waliochukua tuzo mbili za MTV 2014.
Julio Batalia ambaye yuko na Chege Chigunda South Africa alisema….’Kuna collabo inakuja kati ya CHEGE na MAFIKIZOLO, tuombeane kheri  ili tufanye kitu kizuri ambacho kitapendeza na kurepresent Tanzania. Tuendelee kupeana support na tufanye mambo makubwa’Julio alisema

BOFYA  HAPO CHINI UJISHINDIE RANGE ROVER KWA SIKU YA REO..

Sunday

Wiz Kid Kufanya kolabo na R Kelly Pamoja na Alicia Keys...

Wiz Kid Kufanya kolabo na R Kelly Pamoja na Alicia Keys...


Kupitia interview East Africa Radio na Sammisago Wiz Kid baada ya kutua Tanzania kwaajili ya show yake leaders Club Wiz Kid amethibitisha kuwa amefanya wimbo na R Kelly.
Wiz Kid amesema ” R Kelly alimpigia simu na kumtumia wimbo wake ambao alitaka wapige collabo na wimbo huu utakuwepo kwenye album mpya ya  R Kelly, wimbo utakuwa R Kelly ft Wiz Kid “.
” i just did a record with R Kelly…it is a record for his new album ” maneno ya Wiz Kid.
Wiz Kid pia amethibitisha kuwa amerekodi nyimbo tano na rapa Ty Dolla Sign.

Kwenye maongezi ambayo yalikuwa nje ya studio nimepata uthibitisho kuwa baada ya kufanya show ya ‘Keep A Child Alive ‘ ya Alicia Keys, Wiz Kid ataingia studio na Alicia Keys kufanya naye wimbo ambao utakuwa wa Alicia Keys.Keep stay on