Showing posts with label BONGO NEWZ. Show all posts
Showing posts with label BONGO NEWZ. Show all posts

Saturday

V'EE JAY NA PRODUCER WAKE SELF KUWA WAMALIZA TOFAUTI ZAO

V'EE JAY NA PRODUCER WAKE SELF KUWA WAMALIZA TOFAUTI ZAO


V'ee Jay Ni Miongoni Mwa Watanzania Waliopo Nje Ya Nchi Na Anafanya Harakati Za Muziki Nchini Marekani, NiMuda Mrefu Sasa Umepita Toka Waingie Katika Tofauti Na Producer Wake Wa Muda Mrefu Self Kuwa Ambaye Pia Ni C.E.O Wa Lab Ya Ukweli Records,Akizungumza Na MULEBA KWANZA MEDIA 

Self Kuwa Amesema Kuna  Project Nyingi Na Kubwa Ambazo Wana Ziachia Hivi Karibuni Baada Ya Kumaliza Tofauti Zao Na Msanii Wake Vee Jay Ikiwemo Na Collaboration Yake Na Msanii Madee Kutoka Tanzania,
Self Kuwa Amesema Pia Team Nzima Ya Lab Ya Ukweli Na Too CoolMusic Watatambulishwa Katika Tamasha Kubwa La SYRACUSE UNITED & CELEBRATION OF REFUGEE SUCCESS Litakalofanyika SYRACUSE NEW YORK Hivi Karibuni Nchini Marekani.

Sunday

Q Boy Msafi akana kuupinga mtandao wa wasafi.com

Q Boy Msafi akana kuupinga mtandao wa wasafi.com

Msanii wa Bongo Fleva, Q Boy Msafi ambaye alikuwa mbunifu wa mavazi ya Diamond Platnumz amesema si kweli alikuwa anapinga ujio wa mtandao wa wasafi.com kitu kilichopelekea kutimuliwa WCB.

Q Boy ameiambia kipindi cha cha The Play List cha Times FM,  wakati mtandao huo unaanzishwa yeye tayari alikuwa nje ya WCB.
“Suala la wasafi.com hata walipozindua mimi sikuwepo. Hata maandalizi for real nilikuwa mbali na vikao ambavyo walikuwa wanafanya kwa sababu nilikuwa out of wasafi na nilikuwa nimeshanza kufuatilia ishu zangu lakini nilikuwa na fununu kuwa wasafi wanafungua mtandao,” amesema Q Boy.
Katika hatua nyingine Q Boy amesema sababu ya wimbo wake mpya ‘Karorero’ kutokuwepo katika mtandao huo ni kwamba tayari alikuwa ameshauuza kwa watu wengine.
“Wimbo wangu wa pili sikuupeleka ila bosi Tale aliniandikia kwenye Whats App fanya ulete wimbo wako kwenye wasafi .com lakini mimi nilikuwa nimeshakaa chini na watu ambao nilitaka kuwapa caller tunes, so sikuweza kuchanganya,” ameongeza.

Saturday

Zilizotufikia: Roma na wenzake wapatikana wakiwa salama

Zilizotufikia: Roma na wenzake wapatikana wakiwa salama

Taarifa zilizotufikia zimedai kuwa Roma na watu wengine waliokuwa wameshikiliwa tangu Jumatano hii wamepatikana wakiwa salama.
Mkuu wa polisi (OCD) wilaya ya Kinondoni, Abubakar Kunga amethibitisha kupatikana kwa wote waliopotea. Lakini kwa sasa amesema wanafanya nao mahojiano ya kipolisi katika kituo cha Oysterbay lakini baada ya muda mfupi wataongea na waandishi ili kutoa taarifa kamili.
Kupatikana kwao kumefuatia wito mkubwa uliokuwa ukipaishwa na wasanii wenzake na mashabiki kuhusu kuachiliwa huru.
Awali, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishina Simon Sirro alisema bado walikuwa wakiendelea na upelelezi wa tukio la kupotea (kutekwa) kwa msanii Roma Mkatoliki na wenzake.
Akiongea na waandishi wa habari mchana huu Polisi Central jijini Dar es salaam, Kamanda Sirro alisema tukio la utekwaji wa Roma na wenzake ni aina ya matukio ambayo hutokea mara kwa mara.
“Matukio ya utekaji hayajaanza leo, hili la kina Roma na wenzake ni tukio kama matukio mengine yaliyokuwa ya ujambazi kwahiyo tupeni muda tupeleleze, tukifika mahali pazuri tutawaita tuwape taarifa lakini nimeona mitandao mingi inazungumza, jana nikaona wasanii wamekutana lakini nikajiuliza hivi yangekuwa haya matukio yanatokea ya uhalifu yanapotokea watu wanakutana ingekuwaje?,” alisema Sirro.
Aliongeza, “Jamani kazi hii tumepewa kwa mujibu wa Katiba na ni lazima tutimize wajibu wetu kwa hiyo tupeni muda tutakuwa na majibu mazuri katika hili,” aliongeza.
Diamond afafanua sababu za kuachia wimbo ‘Acha Nikae Kimya’ uliogusia suala la Roma

Diamond afafanua sababu za kuachia wimbo ‘Acha Nikae Kimya’ uliogusia suala la Roma

Diamond Platnumz ameachia wimbo wake mpya kwa kushtukiza uitwao ‘Acha Nikae Kimya.’ Wimbo unazungumzia masuala mengi yanayotokea sasa ikiwemo hofu iliyotanda baada ya Roma na wenzie kutekwa.
Wimbo huo hata hivyo umepokelewa kwa hisia tofauti.
Hizi ni sababu zake kwanini ameamua kuuachia:
Ili Nchi ipate maendeleo inahitaji Upendo na Ushirikiano wa Wananchi na Serikali..Na Nikiwa kama Msanii, jukumu langu ni kuhakikisha natumia Hekma na busara kukemea jambo nilionalo haliko sawa ili lirekebishwe, lakini pia panapokuwa hakuna maelewano jukumu langu pia ni kupatanisha ili kwa pamoja tujenge nchi yetu kusudi wazazi wetu, watoto pamoja na familia zetu waishi kwa Upendo Amani na kufurahia nchi yetu…Na ndiomaana kwenye nyimbo nakwambia “MI NA WEWE WA TAIFA MOJA…KAMBARAGE BABA MMOJA….SASA TOFAUTI ZA NINI TUSHIKAMANE TUKAIJENGE TANZANIA”… Unatakiwa utambue kuwa kila kiongozi ni Binadamu na kama wote tujuavyo, Binadamu hatujakamilika… hivyo katika nchi yoyote lazma wakati mwingine kuna jambo linaweza likawa haliko sawa, ila sisi kama wananchi tunatakiwa tutumie Hekima na Busara kwenye kufikisha ujumbe ama hoja zetu ili viongozi walieke sawa…Busara na Hekima itafanya viongozi watuelewe kirahisi na pengine mengi tuyatakayo tutimiziwe kirahisi… mfano mzuri, juzijuzi kupitia kipindi cha Clouds360 cha clouds Tv nlipopata bahati ya kuongea na Mh Raisi nilimuomba atufungulie Mabanda ya Chipsi na Bodaboda ziruhusiwe kufanyakazi hadi asubuhi maana zilikuwa nwisho saa 4 ama 5 usiku…kwakuwa nilitumia Hekima na busara kwenye Kufikisha hoja ama Ombi langu..alikubali na tukapewa ruksa na sasa hivi maeneo mengi ya Chipsi na Bodaboda yanafanya kazi hadi usiku mnene… hivyo tusikubali tu kulishwa Sumu za kuleta ugomvi kati yetu wenyewe kwa wenyewe eti Mara Tutukane mara sijui fanyeni hiki, wakati hata baadhi ya wanaochochea mambo hayo hawaishi Tanzania wanaishi Ulaya / Marekani / kifupi nje ya nchi…ikija kutokea bahati mbaya kimenuka wao watakuwa wanakula kuku kwa mrija huko walipo…halafu sisi na familia zetu ndio tutateseka na kuhaha kunusuru roho zetu usiku kucha.. Hatutaki makelele ya Uchonganishi mitandaoni, kama mtu kweli anauchungu na nchi na kweli akisemacho anamaanisha aje, na kwa pamoja twende sehemu husika kupeleka malalamiko sio kukaa kitandani kupost kuchochea Ugomvi kumbe anatuchora na kutufanya kama sie mataahira wake, anatupeleka mara kushoto mara kulia… Akikaa pekeake anatucheka kuwa sie wajinga wake katueka mkononi…

Sunday

 Nay wa Mitego kukamatwa na polisi ni kutokana na wimbo wake Wapo

Nay wa Mitego kukamatwa na polisi ni kutokana na wimbo wake Wapo

Nay wa Mitego amedai amekamatwa na polisi wilayani Mvomero, Morogoro alikokuwa ameenda kwaajili ya show.
Hajasema sababu ya kukamatwa kwake lakini watu wanahisi ni kutokana na wimbo wake Wapo ambao umemkosoa vikali Rais Dkt John Magufuli. “Nimekamatwa kweli. Muda Huu nikiwa hotel Morogoro baada ya kumaliza Kazi yangu iliyo ni leta. Napelekwa Mvomelo Police,” ameandika rapper huyo mtata.
“Nawapenda Watanzania wote. #Truth #Wapo,” ameongeza.

Monday

Diamond afungua mwaka na deal hii kubwa ya ubalozi

Diamond afungua mwaka na deal hii kubwa ya ubalozi

Msanii wa muziki Nassib Abdul maarufu, Diamond Platnumz ameteuliwa rasmi na kampuni ya GSM kuwa balozi wa kutangaza bidhaa mbalimbali za taasisi hiyo.
Akizungumza Jijini Dar es Salaam Afisa Masoko wa kampuni hiyo, Lauma Mohamed ameeleza kuwa Diamond
Platnumz ni msanii mkubwa sana ndani na nje ya Afrika, hivyo wanaimani atakuwa balozi mzuri kwa bidhaa zao
bora kwa watanzania.
Kwa upande wake Diamond Platnumz ameeleza kuwa anafarijika sana kuona wasanii watanzania wanapata nafasi
ya kuwa mabalozi, kwani wasanii ni wengi lakini yeye amepata heshima hiyo hivyo ana imani ni jambo jema kwa tasnia ya muziki.
Ameongeza kuwa hapo mwanzo bidhaa nyingi kwa mfano samani za ndani zilikuwa zinaagizwa nje ya nchi lakini kwa
sasa itakuwa rahisi kwani GSM kwenye duaka lao la ‘The New Home’ wanauza samani hizo halkadhalika nguo za watoto.
Licha ya kumtambulisha msanii huyo kama balozi mpya wa GSM wamezindua matangazo mapya mawili yaliyoigizwa na msanii
huyo pamoja na familia yake akiwemo Zari the Boss Lady na mtoto wao Tiffa, huku tangazo moja likiwa la nguo na lingine la samani za ndani.

Sunday

Hii ndio sababu ya Temba kukaa kimya kwa muda mrefu kwenye muziki

Hii ndio sababu ya Temba kukaa kimya kwa muda mrefu kwenye muziki

Mh Temba amefunguka sababu ya kukaa kimya kwa muda mrefu kwenye muziki.
Msanii huyo amekiambia kipindi cha FNL cha EATV kuwa alitakiwa kuachia wimbo mpya mapema kabala hata ya ‘Acha Waoane’ wa Chege lakini kuna vitu viliingiliana vikavuruga ratiba hiyo.
Temba amevitaja vitu hivyo ni pamoja na kuibiwa fedha zake na zingine za baadhi ya marafiki zake ambazo alitegemea kufanyia kazi kwenye muziki ikiwemo kutumika kwenye kutengenezea video.
Rapper huyo amemtaja aliyewaibia anaitwa Mustafa Andumbotela Ndingubita na ameahidi kutoa kiasi cha milioni moja kwa mtu atakayesaidia kukamatwa kwake huku naye Chege akiongezea kiasi cha laki tano kwenye zawadi hiyo ambapo itakuwa ni milioni moja na nusu.

Thursday

Diamond: Nikiwa natoa nyimbo, siwazi redio na TV kama sehemu ya promotion

Diamond: Nikiwa natoa nyimbo, siwazi redio na TV kama sehemu ya promotion

Diamond Platnumz amesema kwa sasa redio na TV si vyombo anavyovitegemea sana kwaajili ya promotion pindi anapokuwa akiachia nyimbo.
“Mimi nikiwa natoa nyimbo yangu, promotion yangu siwazi redio wala siwazi TV, ever. Promotion yangu ya kwanza mimi nawaza nyimbo iwafikiaje watu, kuna mitandao ya kijamii, kuna digital platform nyingi,” staa huyo alisema kwenye kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz.
Alidai kuwa zama za kundi Fulani la watu likiamua kumrudisha nyuma msanii, halipo tena kwa wasanii wenye nguvu kama yeye.
“Tufute zile ‘naweza nikamdhuru mtu fulani ninavyotaka mimi’ vile vitu havipo tena,” aliongeza.
Wema aalikwa kwenye 40 ya Prince Nillan Jumamosi hii

Wema aalikwa kwenye 40 ya Prince Nillan Jumamosi hii

Zari na Wema Sepetu mambo mbona fresh tu. Malkia huyo wa filamu nchini amealikwa kwenye sherehe ya 40 ya Prince Nillan.
Wakizungumza kwenye kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM Alhamis hii, Diamond amethibitisha kuwa Wema ni mmoja kati ya wageni walioalikwa katika shughuli hiyo.
“Ni mmoja kati ya watu ambao wamealikwa. Na tunaomba wamalize matatizo yao salama,” amesema Diamond.
Sherehe hiyo inatarajiwa kufanyika Jumamosi ya Februari 11 mwaka huu huko kwenye ikulu ya Diamond na Zari iliyopo Madale.

Monday

Mama Wema Sepetu ashinda Polisi kujua hatima ya mwanaye

Mama Wema Sepetu ashinda Polisi kujua hatima ya mwanaye

Sakata la baadhi ya wasanii wakubwa nchini kuhusishwa na biashara ya dawa za kulevya limezidi kuchukua sura mpya, huku mzazi wa Wema Sepetu akishinda polisi kujua hatima mwanaye.
Akiongea huku akiwa kama mtu aliyepatwa na hamaki mama mzazi wa Wema Sepetu, alisema kwa sasa anasubiri kauli ya Polisi ili aweze kujua kama mtoto wake atafikishwa mahakamani au laa.
Alisema kitendo cha kukamatwa mtoto wake na kuwekwa ndani kimemuumiza kama mzazi ingawa kwa sasa hana la kufanya zaidi ya kusubiri uamuzi wa vyombo vya dola.
“Kama mzazi nimeumia sana ila kwa sasa ninawaomba mniache maana siwezi kuongea kitu chochote kuhusu hili, hadi hapo polisi itakapotoa maamuzi yao ya uchunguzi wanaoufanya, ndiyo nitajua nini niseme,” mama Wema aliliambia gazeti la Mtanzania.
Baada ya kutoa kauli hiyo mama huyo alionekana ni mtu mwenye msongo ambapo muda wote alikuwa amekaa kimya tofauti na ilivyo kawaida yake ambapo huwa ni mtu mwenye uchu.
Tazama Video Ya Diamond Alivoporomosha matusi mazito kwenye Instagram Live

Tazama Video Ya Diamond Alivoporomosha matusi mazito kwenye Instagram Live

Instagram Live inawapa uchizi mastaa na kadri siku zinavyokwenda, mambo yanazidi kuchemka.

Jumapili iliyomalizika, Diamond alikuwa live kwa muda mrefu kwenye mtandao huo akiwa nyumbani kwake, Pretoria, Afrika Kusini pamoja na familia yake. Kwenye video hiyo ya moja kwa moja, kwa wakati fulani Diamond alipewa kampani na mama wa watoto wake, Zari pamoja na mtoto wao wa kwanza, Tiffah.

Hata hivyo mambo yalibadilika baada ya staa huyo kuanza kutokwa na matusi ya nguoni aliyoyaelekeza kwa mtu aliyamuambia kuwa anamchukia. “You don’t need to hate me because I don’t hate you, by the way I don’t f*cking know you, the person that hates me, I don’t know him,” anasikika Diamond kwenye video hiyo. “I only know people who love me because I always concentrate with people who love me, who support me, if you hate me f*ck you, I don’t know you,” lilimchomoka tusi. Aliendelea, “You don’t even stress me out because I know you must be broke, If you are not broke, there is no way you can hate me, if you hate me you’re motherf*cking broke, and if you’re broke you can’t stress me out because I got money more than you, I got cars more than you, I got houses more than you, I got money motherf*cker in the bank more than you. You and your family know that, so if you hate me go to hell.” Alibadilisha lugha, “Nyie mnaonichukia endeleeni kunichukia sababu kila siku nafanya maajabu, mwaka huu ndio nafanya maajabu mengi.” Kama kawaida, video hiyo imepokelewa kwa hisia tofauti huku wengi wakichukizwa na matusi aliyoyatoa.

Sunday

 Alikiba, yazingatie malalamiko ya mashabiki wako

Alikiba, yazingatie malalamiko ya mashabiki wako

Ali Saleh Kiba al maarufu kama Alikiba ni miongoni mwa wasanii wakongwe na wakubwa Tanzania, Afrika Mashariki na pengine Afrika kwa ujumla. Ni mshindi wa tuzo zaidi ya 14 kwa mwaka 2016 ikiwezo tunzo kubwa kabisa za MTV EMA kwa kipengele cha Best African Act.
Kwa mafanikio makubwa aliyoyapata mwaka jana ikiwemo kupata mkataba mnono wa kampuni kubwa ya muziki duniani yaani Sony Music na kushinda tuzo zote hizo ndani ya mwaka 2016 ni wazi kabisa kuwa thamani ya Alikiba imepanda maradufu barani Afrika na pengine kila mfuatiliaji wa muziki Afrika angependa zaidi kumfahamu Alikiba, kufahamu kazi zake, ni wapi ametoka na wapi anakwenda.
Sekeseke lilitokea mwaka jana kwenye show ya Mombasa rocks iliyofanyika mjini Mombasa, Kenya kati ya Wizkid na Alikiba ni moja kati ya mambo ambayo yalifanya jina la Alikiba lizungumzwe sana barani Afrika haswa Tanzania, Kenya na Nigeria ambapo mitandao mbalimbali ya Nigeria iliripoti kua Alikiba anatrend sana nchini Nigeria.
Ushindi wa MTV EMA pia ambao awali alipewa Wizkid kabla haujatenguliwa na kupewa Alikiba ni mambo yaliyofanya apate attention zaidi kwenye soko la muziki barani Afrika.
Kutrend ni kitu muhimu sana katika soko la muziki kwa sasa, wasanii wengi duniani kote hata mpaka Marekani wamekuwa wakitengeneza kiki kabla ya kuachia kazi zao mpya ili kupata attention. Nafahamu kuwa msanii Alikiba amekuwa sio muumini mzuri sana wa kiki, lakini kiki kama hizi ambazo zinajitengeneza zenyewe ni dhambi kubwa kuacha kuzitumia kibiashara sababu kuna wanaotamani kutrend hata kwa kutembea uchi lakini hawazipati.
Mapema mwaka huu Alikiba alitangaza ratiba ya World Tour yake itakayoanzia South Africa kisha America na kumalizikia barani Ulaya. Kwa mujibu wa ratiba kutoka kwenye posters zake alizozipost Instagram Tour yake inaanza February mwaka huu. Hivyo mpaka ninaandika makala hii zimebaki siku tatu kufikia mwezi February.
Kati ya sehemu ngumu sana kupenya kimuziki barani basi ni Afrika Kusini na hii imetokana na ‘wasauzi’ kuthamini sana muziki wao na haikushangaza licha ya jina kubwa alilojijengea Diamond Platnumz kwenye kiwanda cha muziki barani Africa aliwahi kaririwa akisema amefanya collaboration na AKA ili kupenyeza muziki wake África Kusini.
Sasa wasiwasi wangu ni je? Alikiba anategemea kujaza viti kwa kuitegemea nyimbo ya Aje pekee? Target yake kwenye hii tour ni kuifanya iwe ya kidunia au analenga waTanzania pekee wanaoishi kwenye nchi husika? Aliahidi atatoa Aje remix ambayo ni nyimbo aliyoimba na msanii kutoka Nigeria MI Abaga lakini mpaka zimebaki siku tatu kabla hatujaingia mwezi anaoanza tour hakuna dalili ya hiyo nyimbo?
Binafsi nilidhani ingekuWa sahihi sana kama angeachia nyimbo ambayo amesharekodi mama mkongwe Yvonne Chakachaka kwa lengo la kuiteka zaidi South Africa kibiashara zaidi ili jina lake liwe kubwa nchini humo hata wakati wa Tour yake angetumia pia na fursa hiyo kufanya media tour kuitambulisha zaidi hiyo ngoma.
Nadhani si Mimi ila asilimia 98 ya mashabiki hawaridhishwi na namna ambayo Alikiba amekuwa slow sana na kutojua namna soko la mUziki linavyoenda na nini linataka. Ni jana kupitia mtandao wa instagram msanii wa maigizo ambaye pia ni shabiki mkubwa wa msanii Alikiba alipost kipande cha screenshot kikionesha ujumbe aliotumiwa na shabiki mwingine wa Alikiba DM kua Ali atapoteza mashabiki wake sababu hawapi raha wanayoitaka, siku zote amekuwa mtu wa kujiamini na kuwasibirisha mashabiki wake ambao ukweli bila wao asingekua hapo halipo leo.
Mwaka mpya umeanza kwa kasi kweli kila mtu yuko kasi lakini naona Alikiba bado yule yule.

Saturday

 Hii ndio sababu ya Mo Music kuwa ‘single’

Hii ndio sababu ya Mo Music kuwa ‘single’

Mo Music anadai bado yupo single na tayari kumingle.
Mkali huyo kutoka Rock City, kupitia kipindi cha Power Point cha Kings Fm,ameweka wazi sababu ya yeye kutokuwa kwenye mahusiano.
“Wengi wanakupenda kama Mo Music na sio mimi kama mimi. Wanawake wengi sasa hivi wanaangalia watu wenye kitu,lakini ingawa sio wote ila asilimia kubwa,” amesema Mo Music.
Mo Music aliyeanza kufanya vizuri kupitia ngoma yake ya Basi Nenda, kwa sasa ana wimbo uitwao Ado Ado alioutoa mwaka jana.

Thursday

Kajala akanusha binti yake kuharibikiwa kimaadili, ni baada ya video chafu inayodaiwa ya Paula kusambaa mtandaoni

Kajala akanusha binti yake kuharibikiwa kimaadili, ni baada ya video chafu inayodaiwa ya Paula kusambaa mtandaoni

Katika mitandao mbalimbali ya kijamii ipo video iliyosambaa ambayo inamuhusu binti mdogo wa chini ya miaka 18 akifanya mapenzi na mtu mzima ndani ya Gari.
Kijala na binti yake Paula
Awali ilisemekana kuwa katika video hiyo binti aliyeonekana ni Paula Paul ambaye ni mtoto wa staa wa filamu Kajala Masanja hali ambayo ilimfanya muigizaji huyo kukanusha uvumi huyo.
Muigizaji huyo kupitia instagram ameandika:
Hey everyone….jamani mimi sina shida na mtu kama akinichukia au akinisema mimi kwa kitu chochote kile…kwasababu najua binadamu kuongea mmezoea..ila katika kuongea kwenu,kuingilia na kujudge my life naomba msimuingize mtoto wangu…sijawahi kumuomba mtu anisaidie kulea hata siku moja…mimi nimeona kuna video insambaa mnasema ni mwanangu na mnajua kabisa sie paula huyo ila ilimradi tu mfurahishe roho zenu…nilinyamaza…ila sasa naona mnakoelekea ni pabaya..mnahisi yeye hana moyo? Au mnahisi haumii?.mwanangu anasoma na sitaki mumchanganye na mambo yenu ya kipuuzi…vitu vibaya mnavyo muombea mwanangu viwarudie wenyewe…leave my daughter alone jamani…give us a break..fanyani tu mambo yenu yatakayofanya mpate faida katika maisha”,
Mpenzi wa Ray Kigosi, Chuchu Hans ajifungua mtoto wa kiume

Mpenzi wa Ray Kigosi, Chuchu Hans ajifungua mtoto wa kiume

Mpenzi wa msanii mkongwe wa filamu Ray Kigosi, Chuchu Hans amejifungua mtoto wa kiume wiki hii, Ray amethibitisha.
Ray alipost picha kuonyesha sehemu ya mwili ya mtoto wake
Muigizaji huyo ameonyesha furaha yake kwa kuwa huyo ni mtoto wake wa kwanza.
“Asante mungu kwa kuniletea pacha wangu asante my lovely mzungu kwa kunipa heshima kubwa kunifanya niitwe baba, mungu wangu wa haki asiyeshindwa na jambo akubariki sana,” muigizaji huyo aliandika Instagram.
Aliongeza, “Sasa msianze maneno yenu kwamba mwanangu amekunnywa maji, mtoto bado ni mchanga maana watu wa Insta kiboko lakini hawaishi mtoni,”
Kwa upande wa Chuchu Hans huyo ni mtoto wake wa pili, mtoto wake wa kwanza alizaa na mume wake wa zamani.

Wednesday

 Izzo Bizness: Chidi Benz alinisaidia sana kiuchumi kipindi nimefulia

Izzo Bizness: Chidi Benz alinisaidia sana kiuchumi kipindi nimefulia

Nimewahi kuzungumza na Ditto kwa ufupi na akanieleza kuwa katika watu wenye roho nzuri katika kusaidia watu, Chidi Benz ni namba moja.
Alisema kipindi ambacho rapper huyo ana fedha, washkaji wengi wa karibu yake walifaidika sababu hana tabia ya uchoyo. Izzo Bizness amekiri kuwa mmoja wa watu walionufaika na ukarimu wa Chidi Benz.
“Hata mimi wakati sina kitu yaani, unakuta unampigia simu [Chidi Benz] ‘ebana eh inakuaje uko wapi? Hebu njoo tukutane Ubungo.’ Unaenda unachezea labda shilingi 50 fulani, shilingi 30,” alisema Izzo kwenye mahojiano na kipindi cha The Playlist cha Times FM.
Izzo anadai kuwa pamoja na misaada ya kifedha ya hapa na pale, Chidi alikuwa mtu aliyekuwa akimpa ushauri mwingi uliomjenga kimuziki.
“Chidi atabaki kuwa big brother, kuna mambo ya duniani kila mtu ana mitihani yake lakini hata mimi namuombea, nammiss, game imepoa Chidi ni bonge ya rapper, hamna ambaye hajui, kuna vijana wengi sana ametusaidia,” amesisitiza Izzo.
 WCB ya Diamond kumsaini Q Chief?

WCB ya Diamond kumsaini Q Chief?

Label kubwa ya muziki nchini, WCB ya Diamond Platnumz, huwenda ikamsaini msanii mkongwe wa muziki nchini Q Chief.
Muimbaji huyo aliyewahi kufanya vizuri na wimbo ‘Si Ulinikataa’ hivi karibuni alitembelea katika ofisi za WCB na kufanya mazungumzo na uongozi wa label hiyo.
Akiongea katika kipindi cha Yaliyomoyamo cha Radio One Stereo Jumatano hii, Q Chief amedai hivi karibuni alikuwa kwenye mazungumzo la label kubwa ya muziki nchini Tanzania.
“Tayari nimenza kuyaa approach makampuni makubwa sana,” alisema Q Chief. “Kuna uwezokano nikasaini na mmoja ya wadogo zangu ambaye anafanya vizuri kuliko msanii yeyote hapa nchini,”
Aliongeza, “Lakini si nasaini kwa sababu mimi ni mjinga, nasaini kwa sababu nataka kuudhihirisha mimi ni Abubakar Katwila na hakunaga Abubakar Katwila mwingine,”
Muimbaji huyo kwa sasa anafanya vizuri wa wimbo Sungura.

Friday

Nay wa Mitego: MR T Touch bado ni producer mzuri lakini…

Nay wa Mitego: MR T Touch bado ni producer mzuri lakini…

Nay wa Mitego na producer aliyemtambulisha kwenye game, Mr T Touch walikuwa na chemistry ya aina yake na walifanikiwa kutengeneza hits nyingi.
Baada ya kufanya kazi kwa muda katika studio za Free Nation za Nay, Touch aliamua kujiengua na kwenda kuanzisha studio yake mwenyewe. Huko bado anaendelea kufanya vizuri. Pamoja na kwamba hawafanyi tena kazi pamoja, Nay anakiri kuwa Touch bado ni producer mzuri.
“Ni producer mzuri, nimefanya naye kazi kwa muda mrefu so sidhani kama kutakuwa na kitu kipya cha ajabu toka kwake,” Nay alimuambia mtangazaji wa Kings FM, Prince Ramalove.
Hata hivyo Nay anadai tangu aondoke Free Nation bado hajasikiliza ngoma mpya za producer huyo.

Saturday

Solo Thang: Sikuwa na nia ya kumdhalilisha Chidi Benz

Solo Thang: Sikuwa na nia ya kumdhalilisha Chidi Benz

Msanii mkongwe wa muziki wa Hip Hop nchini, Solo Thang amefunguka baada ya baadhi ya watu kumjia juu kwa kusambaza kipande cha video alichorekedi akiwa na Chidi Benz.
Akiongea kwenye kipindi cha E News cha EATV, Solo amesema kuwa Chidi ndiye aliyemtaka amshoot video wakati walipokutana ila hakuwa na nia kama watu wengine wanavyofikiria.
“Chidi ni mdogo wa rafiki yangu na nilimfahamu zamani sana kabla hata hajaanza kuimba. Hivyo tuna historia ndefu kidogo. Chid kwa sasa huwa hapigi picha na watu, lakini tulipoonana ni yeye mwenyewe ndiye alitaka tushoot ile video lakini sikuwa na nia ya kumchoresha,” amesema Solo.
Rapper huyo ameongeza kuwa watu waache kumlaumu Chidi kwa kile kilichomtokea na badala yake wanatakiwa kumpatia msaada bila ya kuchoka.

Thursday

 Mpenzi mpya wa Shilole: Mimi kuchora tattoo ya Shilole ni moyo wangu tu umetaka kufanya hivi

Mpenzi mpya wa Shilole: Mimi kuchora tattoo ya Shilole ni moyo wangu tu umetaka kufanya hivi

Mpenzi mpya wa Shilole ambaye ni mfanyabiashara wa nguo, Adam, amefunguka na kuzungumzia jinsi wanavyopendana na Shilole.
Kijana huyo alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio kuwa hamwangalii Shilole alipotoka bali anaangalia hapo alipo kwa sasa na anamuomba sana Mungu ili waweze kufika mbali zaidi.
“Mimi sijafuata boost kwa Shilole bali nimefuata mapenzi na mimi naweza kusema kuwa hayo ya nyuma siyaangalii bali naangalia hapa tulipo,” alisema Adam
Aliongeza “Kwa sasa na mimi kuchora tattoo ni moyo wangu tu umetaka mimi kufanya hivi, na ninachomuomba Mungu ni kufika mbali tu na yeye basi,”
Hapo awali Shilole kabla ya kuingia kwenye mahusiano na kijana huyo alikuwa anatoka na msanii chipukizi wa muziki aitwae Hamadai.