Showing posts with label BONGO NEWZ. Show all posts
Showing posts with label BONGO NEWZ. Show all posts

Saturday

V'EE JAY NA PRODUCER WAKE SELF KUWA WAMALIZA TOFAUTI ZAO

V'EE JAY NA PRODUCER WAKE SELF KUWA WAMALIZA TOFAUTI ZAO


V'ee Jay Ni Miongoni Mwa Watanzania Waliopo Nje Ya Nchi Na Anafanya Harakati Za Muziki Nchini Marekani, NiMuda Mrefu Sasa Umepita Toka Waingie Katika Tofauti Na Producer Wake Wa Muda Mrefu Self Kuwa Ambaye Pia Ni C.E.O Wa Lab Ya Ukweli Records,Akizungumza Na MULEBA KWANZA MEDIA 

Self Kuwa Amesema Kuna  Project Nyingi Na Kubwa Ambazo Wana Ziachia Hivi Karibuni Baada Ya Kumaliza Tofauti Zao Na Msanii Wake Vee Jay Ikiwemo Na Collaboration Yake Na Msanii Madee Kutoka Tanzania,
Self Kuwa Amesema Pia Team Nzima Ya Lab Ya Ukweli Na Too CoolMusic Watatambulishwa Katika Tamasha Kubwa La SYRACUSE UNITED & CELEBRATION OF REFUGEE SUCCESS Litakalofanyika SYRACUSE NEW YORK Hivi Karibuni Nchini Marekani.

Sunday

Q Boy Msafi akana kuupinga mtandao wa wasafi.com

Q Boy Msafi akana kuupinga mtandao wa wasafi.com

Msanii wa Bongo Fleva, Q Boy Msafi ambaye alikuwa mbunifu wa mavazi ya Diamond Platnumz amesema si kweli alikuwa anapinga ujio wa mtandao wa wasafi.com kitu kilichopelekea kutimuliwa WCB.

Q Boy ameiambia kipindi cha cha The Play List cha Times FM,  wakati mtandao huo unaanzishwa yeye tayari alikuwa nje ya WCB.
“Suala la wasafi.com hata walipozindua mimi sikuwepo. Hata maandalizi for real nilikuwa mbali na vikao ambavyo walikuwa wanafanya kwa sababu nilikuwa out of wasafi na nilikuwa nimeshanza kufuatilia ishu zangu lakini nilikuwa na fununu kuwa wasafi wanafungua mtandao,” amesema Q Boy.
Katika hatua nyingine Q Boy amesema sababu ya wimbo wake mpya ‘Karorero’ kutokuwepo katika mtandao huo ni kwamba tayari alikuwa ameshauuza kwa watu wengine.
“Wimbo wangu wa pili sikuupeleka ila bosi Tale aliniandikia kwenye Whats App fanya ulete wimbo wako kwenye wasafi .com lakini mimi nilikuwa nimeshakaa chini na watu ambao nilitaka kuwapa caller tunes, so sikuweza kuchanganya,” ameongeza.

Saturday

Zilizotufikia: Roma na wenzake wapatikana wakiwa salama

Zilizotufikia: Roma na wenzake wapatikana wakiwa salama

Taarifa zilizotufikia zimedai kuwa Roma na watu wengine waliokuwa wameshikiliwa tangu Jumatano hii wamepatikana wakiwa salama.
Mkuu wa polisi (OCD) wilaya ya Kinondoni, Abubakar Kunga amethibitisha kupatikana kwa wote waliopotea. Lakini kwa sasa amesema wanafanya nao mahojiano ya kipolisi katika kituo cha Oysterbay lakini baada ya muda mfupi wataongea na waandishi ili kutoa taarifa kamili.
Kupatikana kwao kumefuatia wito mkubwa uliokuwa ukipaishwa na wasanii wenzake na mashabiki kuhusu kuachiliwa huru.
Awali, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishina Simon Sirro alisema bado walikuwa wakiendelea na upelelezi wa tukio la kupotea (kutekwa) kwa msanii Roma Mkatoliki na wenzake.
Akiongea na waandishi wa habari mchana huu Polisi Central jijini Dar es salaam, Kamanda Sirro alisema tukio la utekwaji wa Roma na wenzake ni aina ya matukio ambayo hutokea mara kwa mara.
“Matukio ya utekaji hayajaanza leo, hili la kina Roma na wenzake ni tukio kama matukio mengine yaliyokuwa ya ujambazi kwahiyo tupeni muda tupeleleze, tukifika mahali pazuri tutawaita tuwape taarifa lakini nimeona mitandao mingi inazungumza, jana nikaona wasanii wamekutana lakini nikajiuliza hivi yangekuwa haya matukio yanatokea ya uhalifu yanapotokea watu wanakutana ingekuwaje?,” alisema Sirro.
Aliongeza, “Jamani kazi hii tumepewa kwa mujibu wa Katiba na ni lazima tutimize wajibu wetu kwa hiyo tupeni muda tutakuwa na majibu mazuri katika hili,” aliongeza.
Diamond afafanua sababu za kuachia wimbo ‘Acha Nikae Kimya’ uliogusia suala la Roma

Diamond afafanua sababu za kuachia wimbo ‘Acha Nikae Kimya’ uliogusia suala la Roma

Diamond Platnumz ameachia wimbo wake mpya kwa kushtukiza uitwao ‘Acha Nikae Kimya.’ Wimbo unazungumzia masuala mengi yanayotokea sasa ikiwemo hofu iliyotanda baada ya Roma na wenzie kutekwa.
Wimbo huo hata hivyo umepokelewa kwa hisia tofauti.
Hizi ni sababu zake kwanini ameamua kuuachia:
Ili Nchi ipate maendeleo inahitaji Upendo na Ushirikiano wa Wananchi na Serikali..Na Nikiwa kama Msanii, jukumu langu ni kuhakikisha natumia Hekma na busara kukemea jambo nilionalo haliko sawa ili lirekebishwe, lakini pia panapokuwa hakuna maelewano jukumu langu pia ni kupatanisha ili kwa pamoja tujenge nchi yetu kusudi wazazi wetu, watoto pamoja na familia zetu waishi kwa Upendo Amani na kufurahia nchi yetu…Na ndiomaana kwenye nyimbo nakwambia “MI NA WEWE WA TAIFA MOJA…KAMBARAGE BABA MMOJA….SASA TOFAUTI ZA NINI TUSHIKAMANE TUKAIJENGE TANZANIA”… Unatakiwa utambue kuwa kila kiongozi ni Binadamu na kama wote tujuavyo, Binadamu hatujakamilika… hivyo katika nchi yoyote lazma wakati mwingine kuna jambo linaweza likawa haliko sawa, ila sisi kama wananchi tunatakiwa tutumie Hekima na Busara kwenye kufikisha ujumbe ama hoja zetu ili viongozi walieke sawa…Busara na Hekima itafanya viongozi watuelewe kirahisi na pengine mengi tuyatakayo tutimiziwe kirahisi… mfano mzuri, juzijuzi kupitia kipindi cha Clouds360 cha clouds Tv nlipopata bahati ya kuongea na Mh Raisi nilimuomba atufungulie Mabanda ya Chipsi na Bodaboda ziruhusiwe kufanyakazi hadi asubuhi maana zilikuwa nwisho saa 4 ama 5 usiku…kwakuwa nilitumia Hekima na busara kwenye Kufikisha hoja ama Ombi langu..alikubali na tukapewa ruksa na sasa hivi maeneo mengi ya Chipsi na Bodaboda yanafanya kazi hadi usiku mnene… hivyo tusikubali tu kulishwa Sumu za kuleta ugomvi kati yetu wenyewe kwa wenyewe eti Mara Tutukane mara sijui fanyeni hiki, wakati hata baadhi ya wanaochochea mambo hayo hawaishi Tanzania wanaishi Ulaya / Marekani / kifupi nje ya nchi…ikija kutokea bahati mbaya kimenuka wao watakuwa wanakula kuku kwa mrija huko walipo…halafu sisi na familia zetu ndio tutateseka na kuhaha kunusuru roho zetu usiku kucha.. Hatutaki makelele ya Uchonganishi mitandaoni, kama mtu kweli anauchungu na nchi na kweli akisemacho anamaanisha aje, na kwa pamoja twende sehemu husika kupeleka malalamiko sio kukaa kitandani kupost kuchochea Ugomvi kumbe anatuchora na kutufanya kama sie mataahira wake, anatupeleka mara kushoto mara kulia… Akikaa pekeake anatucheka kuwa sie wajinga wake katueka mkononi…

Sunday

 Nay wa Mitego kukamatwa na polisi ni kutokana na wimbo wake Wapo

Nay wa Mitego kukamatwa na polisi ni kutokana na wimbo wake Wapo

Nay wa Mitego amedai amekamatwa na polisi wilayani Mvomero, Morogoro alikokuwa ameenda kwaajili ya show.
Hajasema sababu ya kukamatwa kwake lakini watu wanahisi ni kutokana na wimbo wake Wapo ambao umemkosoa vikali Rais Dkt John Magufuli. “Nimekamatwa kweli. Muda Huu nikiwa hotel Morogoro baada ya kumaliza Kazi yangu iliyo ni leta. Napelekwa Mvomelo Police,” ameandika rapper huyo mtata.
“Nawapenda Watanzania wote. #Truth #Wapo,” ameongeza.