Saturday

V'EE JAY NA PRODUCER WAKE SELF KUWA WAMALIZA TOFAUTI ZAO

V'EE JAY NA PRODUCER WAKE SELF KUWA WAMALIZA TOFAUTI ZAO


V'ee Jay Ni Miongoni Mwa Watanzania Waliopo Nje Ya Nchi Na Anafanya Harakati Za Muziki Nchini Marekani, NiMuda Mrefu Sasa Umepita Toka Waingie Katika Tofauti Na Producer Wake Wa Muda Mrefu Self Kuwa Ambaye Pia Ni C.E.O Wa Lab Ya Ukweli Records,Akizungumza Na MULEBA KWANZA MEDIA 

Self Kuwa Amesema Kuna  Project Nyingi Na Kubwa Ambazo Wana Ziachia Hivi Karibuni Baada Ya Kumaliza Tofauti Zao Na Msanii Wake Vee Jay Ikiwemo Na Collaboration Yake Na Msanii Madee Kutoka Tanzania,
Self Kuwa Amesema Pia Team Nzima Ya Lab Ya Ukweli Na Too CoolMusic Watatambulishwa Katika Tamasha Kubwa La SYRACUSE UNITED & CELEBRATION OF REFUGEE SUCCESS Litakalofanyika SYRACUSE NEW YORK Hivi Karibuni Nchini Marekani.

Sunday

 kauli ya Zitto Kabwe baada ya uteuzi wa Anna Mghwira

kauli ya Zitto Kabwe baada ya uteuzi wa Anna Mghwira

Baada ya uteuzi wa Rais Magufuli jana wa Mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo, Anna Mghwira kuwa mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kulikuwa na mijadala mizito mitandaoni na hata kwenye vyombo vya habari juu ya uteuzi huo huku wengi wakimtaka Mbunge pekee wa chama hicho, Zitto Kabwe atolee ufafanuzi juu uteuzi huo hatimae leo ametoa kauli yake ya kwanza kuhusu uteuzi huo.
Tokeo la picha la zitto Kabwe na anna mghwira
Zitto Kabwe akiteta jambo na Mama Anna Mghwira
Zitto Kabwe amesema amezipokea taarifa hizo kutoka mitandaoni na kwenye vyombo vya habari lakini bado Chama cha ACT wazalendo hakijafanya mawasiliano na Mghwira anmbaye yupo nje ya nchi mpaka atakaporejea ndipo chama kitatoa msimamo wake juu ya uteuzi huo.
Nimekuwa naulizwa Sana kuhusu uteuzi wa Mwenyekiti wa Chama chetu kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Nimekuwa kimya Kwa sababu tumepokea Taarifa za uteuzi kutoka katika vyombo vya Habari. Mwenyekiti yuko nje ya nchi na kutokana na tofauti za masaa bado hatujawasiliana nae. Tutatoa tamko kamili atakapokuwa amerejea nchini.“ameandika Zitto Kabwe kwenye ukurasa wake wa Facebook.
Hata hivyo Zitto Kabwe amewataka Wanachama wa chama cha ACT wazalendo luwa watulivu kwa kipindi hiki mpaka hapo taarifa rasmi itakapotolewa pindi atakaporejea nchini.
Ninawataka wanachama wote wa Act Wazalendo wawe watulivu na Kama kuna masuala yanayohusu maamuzi ya vikao vya Chama tutawajulisha.“ameandika Zitto Kabwe.
Nafasi za kazi Stanbic Bank Tanzania Ltd, Graduate Program

Nafasi za kazi Stanbic Bank Tanzania Ltd, Graduate Program

Stanbic Bank Tanzania Ltd would like to take this opportunity to inform you that we have officially launched our Stanbic Graduate Program. The program is geared towards identifying talented graduates, from all disciplines, who will go through rigorous and robust screening process, with the aim of grooming them to competent bankers.
Job Purpose
Graduate
Key Responsibilities/Accountabilities
Graduate
Preferred Qualification and Experience
Bachelor Degree with Hons (First Class or Upper Second)
Masters Degree
Knowledge/Technical Skills/Expertise
Good writing skills
Strong communication
Confident
Hard Working
Desire to Learn
Computer Literate
APPLY ONLINE
Jobs at Musoma Water Supply and Sanitation Authority (MUWASA)

Jobs at Musoma Water Supply and Sanitation Authority (MUWASA)


VACANCIES
Musoma Water Supply and Sanitation Authority (MUWASA) is an utility established under section 9 of the Water Supply and Sanitation Act No. 12 of 2009 with the objective of provision of Water Supply and Sanitation services in Musoma Municipality. In this respect, the activities of MUWASA have specifically expanded and the authority now invites application from suitably qualified and skilled individuals who are dynamic and result oriented to fill the following posts:
0:1 Job Position: Information Technology Officer I (1 Post)
1 :1 Reporting to: Managing Director
1 :2 Duties and Responsibilities
i. To conduct system analysis related to computer applications.
ii. To design moderately complicated systems on the basis of systems analysis documents.
iii. To write detailed systems specifications related to moderately complicated applications.
iv. To conduct Systems analysis relating to computer applications.
v. To coordinate the data synchronization activities between the engineering and the billing departments.
vi. To manage the meter management billing system and data updating activities.
vii. To make regular back-ups to safeguard both Auto CAD and billing databases
viii. To performing any other duties that may be assigned by the Supervisor.
ix. To plan design and develop system related computer system and programming
1 :3 Minimum Qualifications
Holder of Bachelor Degree or Advanced Diploma in Computer Science, Computer Engineering, Information Communication Technology, Information Systems Analysis, Electronics and Communications from a recognized Institution,
1.4 Minimum Experience
Possession of at least Five (5) years of working in similar field.
1 :5 Age limit
Not above 45 years of age
===========
2:0 Job Position: Customer Relation Officer I 1 Post
2:1 Reporting to: Commercial Manager
2:2 Duties and Responsibilities
i. To identify customers and their needs.
ii. To prepare and develop market plans and programmes.
iii. To monitor and review business performance.
iv. To gather marketing information.
v.To process promotional materials as requested by departments and sections.
vi. To monitor sponsorship and donation requests.
vii. To monitor and maintain promotional materials.
viii. To maintain good customer service when dealing with internal and external customers.
ix. To follow up on supplies of promotional materials
x. To perform any other duties as may be assigned.
2:3 Minimum Qualifications
Holder of Bachelor Degree or Advanced Diploma qualifications in Marketing, Business Administration, Commerce, Mass Communication or related disciplines from recognized Institution, Possession of Master's Degree is an added advantage. He or She must be computer literate.
2.4 Minimum Experience
Possession of at least five (5) years of working in similar field.
2:5 Age limit
Not above 45 years of age
2:6 Remuneration
Active package and fringe benefits as per MUWASA's incentives scheme will be offered to the successful candidates.
Mode of Application
Only qualified persons should submit their handwritten letters of application with certified copies of relevant academic and professional certificates and testimonials so as to reach the undersigned not later than 21st June, 2017. Applicants are also required to indicate the names and contacts of at least three (3) work/professional related referees. Women are encouraged to apply. Only short listed candidates will be informed for interview.
The Managing Director
Musoma Water Supply and Sanitation Authority,
P. 0. Box 233,
MUSOMA.
Q Boy Msafi akana kuupinga mtandao wa wasafi.com

Q Boy Msafi akana kuupinga mtandao wa wasafi.com

Msanii wa Bongo Fleva, Q Boy Msafi ambaye alikuwa mbunifu wa mavazi ya Diamond Platnumz amesema si kweli alikuwa anapinga ujio wa mtandao wa wasafi.com kitu kilichopelekea kutimuliwa WCB.

Q Boy ameiambia kipindi cha cha The Play List cha Times FM,  wakati mtandao huo unaanzishwa yeye tayari alikuwa nje ya WCB.
“Suala la wasafi.com hata walipozindua mimi sikuwepo. Hata maandalizi for real nilikuwa mbali na vikao ambavyo walikuwa wanafanya kwa sababu nilikuwa out of wasafi na nilikuwa nimeshanza kufuatilia ishu zangu lakini nilikuwa na fununu kuwa wasafi wanafungua mtandao,” amesema Q Boy.
Katika hatua nyingine Q Boy amesema sababu ya wimbo wake mpya ‘Karorero’ kutokuwepo katika mtandao huo ni kwamba tayari alikuwa ameshauuza kwa watu wengine.
“Wimbo wangu wa pili sikuupeleka ila bosi Tale aliniandikia kwenye Whats App fanya ulete wimbo wako kwenye wasafi .com lakini mimi nilikuwa nimeshakaa chini na watu ambao nilitaka kuwapa caller tunes, so sikuweza kuchanganya,” ameongeza.
NAFASI YA AJIRA TPC LIMITED, JUNE 2017

NAFASI YA AJIRA TPC LIMITED, JUNE 2017


VACANCY ANNOUNCEMENT
TPC Ltd is one of the fast growing sugar producing companies in Tanzania. The company is situated at the foot of Mount Kilimanjaro. 22 kms south of Moshi Municipality
Applications are invited from energetic, proactive and dynamic Tanzanians to fill vacant position in the Corporate Affairs Department.
POST: 1. RADIOGRAPHER(1Post)
1.0 Reports to the Hospital Manager
1.1 Core Job Description: To deal with day to day Radiographer duties and responsibilities.
1.2 Key Accountabilities
1.2.1 Preparing examination rooms, positioning patients for imaging exams.
1.2.2 Assessing and monitoring patients through treatment and follow-up.
1.2.3 Working closely with medical specialists to plan treatment of tissues defects.
1.2.4 Screening of abnormalities.
1.2.5 Producing and interpreting high quality images of the body to identify and diagnose injury and disease.
1.2.6 Asses patients and their requirements towork out which radiographic techniques to use.
1.2.7 Take responsibilities for radiation safety in your work area, including checking equipment for malfunctions and errors.
1.2.8 Manage referrals to ensure patients receive radiation dose as low as reasonable possible.
1.2.9 Supervising staff and patients in radiation work areas.
1.2.10 Provide support and reassurance to patience, taking into account their physical and psychological needs.
1.2.11 Documenting information with computers.
1.3 Core Competencies
Should demonstrate ability to provide high quality diagnostic imaging services, planning and giving treatment using x-rays and other radioactive resources.
1.4 Personal Specifications
Diploma in Diagnostic Radiography with Sonography must be registered by Tanganyika Medical Imaging and Radiology Council. A combination of relevant certified academic certificates. He/she must possess computer skills and should have at least 2 years working experience.
MODE OF APPLICATION
Candidates meeting the requisite qualifications should submit their written applications and detailed CV to the address below. describing how they see themselves qualifying for this position. They should also send certified copies of academic certificates, three references. daytime telephone numbers and e-mail addresses. The closing deadline for all applications is 16 June, 2017. Any application letter after the deadline will not be considered.
Only shortlisted candidates will be contacted
Human Resources Executive Officer, 
P. 0. Box 93, 
Moshi, Kilimanjaro
Tel: +255272754389, FAX:+255272754391
E-mail:'tpc@tpc.co.tz

Saturday

Spika ana mamlaka kisheria ya kuomba vyombo vya dola kumsaidia kumkamata mtu – Mdee

Spika ana mamlaka kisheria ya kuomba vyombo vya dola kumsaidia kumkamata mtu – Mdee

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee amesema Spika ana mamlaka ya kisheria ya kuomba vyombo vingine vya dola kumsaidia kumkamata mtu huku akisema kuwa ameamua kuwahi Dodoma kuepuka kukomolewa na Spika Ndugai aliyeagiza afike mbele ya Kamati ya Maadili jana asubuhi na kuagiza polisi wamsake popote alipo, ikiwezekana apelekwe akiwa amefungwa pingu.
Mdee, ambaye alikuwa Dar es Salaam wakati amri hiyo ikitolewa juzi saa 5:00 asubuhi, aliwasili Dodoma jana, lakini suala lake litajadiliwa leo. “Spika ana mamlaka ya kisheria ya kuomba vyombo vingine vya dola kumsaidia kumkamata mtu,” alisema Mdee alipoongea na gazeti la Mwananchi.
“Kwa sababu hiyo, ana uwezo wa kutumia mamlaka hayo kumkomoa mtu. Ndiyo maana nikaja mwenyewe Dodoma. Niliacha majukumu mazito niliyokuwa nayo ili lengo lake la kunikomesha lisifanikiwe,” aliongeza. Spika Ndugai, aliyezungumza kwa ukali, alisema anajua kuwa Mdee alikuwa nje ya Dodoma, lakini akataka awe amefika mbele ya kamati hiyo jana muda sawa na ule aliokuwa akitoa maagizo hayo juzi.
Mdee anatuhumiwa kutoa lugha mbaya kwa Spika, Rais na wabunge wakati wa mjadala uliokuwa mkali wa nafasi za wagombea wa Chadema na CUF katika Bunge la Afrika Mashariki.
Mdee pamoja na Kiongozi wa Kambi Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kufika watahojiwa na kamati hiyo leo.
Zilizotufikia: Roma na wenzake wapatikana wakiwa salama

Zilizotufikia: Roma na wenzake wapatikana wakiwa salama

Taarifa zilizotufikia zimedai kuwa Roma na watu wengine waliokuwa wameshikiliwa tangu Jumatano hii wamepatikana wakiwa salama.
Mkuu wa polisi (OCD) wilaya ya Kinondoni, Abubakar Kunga amethibitisha kupatikana kwa wote waliopotea. Lakini kwa sasa amesema wanafanya nao mahojiano ya kipolisi katika kituo cha Oysterbay lakini baada ya muda mfupi wataongea na waandishi ili kutoa taarifa kamili.
Kupatikana kwao kumefuatia wito mkubwa uliokuwa ukipaishwa na wasanii wenzake na mashabiki kuhusu kuachiliwa huru.
Awali, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishina Simon Sirro alisema bado walikuwa wakiendelea na upelelezi wa tukio la kupotea (kutekwa) kwa msanii Roma Mkatoliki na wenzake.
Akiongea na waandishi wa habari mchana huu Polisi Central jijini Dar es salaam, Kamanda Sirro alisema tukio la utekwaji wa Roma na wenzake ni aina ya matukio ambayo hutokea mara kwa mara.
“Matukio ya utekaji hayajaanza leo, hili la kina Roma na wenzake ni tukio kama matukio mengine yaliyokuwa ya ujambazi kwahiyo tupeni muda tupeleleze, tukifika mahali pazuri tutawaita tuwape taarifa lakini nimeona mitandao mingi inazungumza, jana nikaona wasanii wamekutana lakini nikajiuliza hivi yangekuwa haya matukio yanatokea ya uhalifu yanapotokea watu wanakutana ingekuwaje?,” alisema Sirro.
Aliongeza, “Jamani kazi hii tumepewa kwa mujibu wa Katiba na ni lazima tutimize wajibu wetu kwa hiyo tupeni muda tutakuwa na majibu mazuri katika hili,” aliongeza.
mashairi ya wimbo wa Diamond ‘Acha Nikae Kimya’

mashairi ya wimbo wa Diamond ‘Acha Nikae Kimya’

Diamond amepiga style za Beyonce, kuachia ngoma kwa kushtukiza. Wimbo huo uitwao Acha Nikae Kimya unazidi kwenda viral kutokana na ujumbe uliomo ikiwemo kumtetea mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Kama bado hujausikia, haya ni mashairi yake niliyokuandikia:
Nasema walau nina kidogo na mashabiki wananiambia mbona hausemi chochote
Ah, si uko nao siku zote ama ulezi unafanya uogope
Ah na media pande zote wanalalama kiongozi atoke
Ah nchi inaingia matope niende wapi na mimi mtoto wa wote,
Yaani lawama, acha nikae kimya, niongee, kimya (ooh ninyamaze mimi)
Nikae kimya nisemee (kimya) mama kaniambia (acha nikae kimya)
Ooh nifunge m[u]domo, mimi bado m[u]dogo nisiseme (kimya)
Verse
Ni mengi majaribu najaribu kuepuka yasije nicost
Japo mengine swadakta mengine hayana maana
Rafiki kipenzi wa karibu hata nyimbo yake sikuweza ipost
Ila alipokamatwa iliniumiza sana mitandaoni kila kona
Uongo na ukweli unashonwa kila nyumba inanong’ona, ahh, ooh Tanzania
Mara kibembe Dodoma wabunge pinzani wamegoma juzi akapotea na Roma
Ohh Tanzania
Najaribu kunyamaza Makame hataki ohh ananiambia walau nina kidogo
Nyumbani nafungwa geti niende kwa Mangi kununua super gate
Napewa za chini ya kapeti kuna redio imevamiliwa eti
Ehh, napita kwenye magazeti nakuta lundo la watu wameketi
Ehh badala ya kutafuta senti wanabishana tu mambo ya vyeti
Acha nikae kimya (nisiongee ) nikae kimya (ninyamaze kabisa)
Nikae kimya (ulimi koma) kimya (usije kuniponza) acha nikae kimya
(nifunge bakuli langu) nikae kimya (nikojoe nikalale) kimya
Mimi bado mdogo sana mama kanimbia
Bridge
Najiuliza wapi (wapi) najiuliza wapiii, tunakwenda wapi
Wapi, kila siku maneno, wapii, hatuwajengi jamaa
Mimi na wewe ni taifa moja, Kambarage baba mmoja
Sasa tofauti za nini tushikamane tukaijenge Tanzania
Diamond afafanua sababu za kuachia wimbo ‘Acha Nikae Kimya’ uliogusia suala la Roma

Diamond afafanua sababu za kuachia wimbo ‘Acha Nikae Kimya’ uliogusia suala la Roma

Diamond Platnumz ameachia wimbo wake mpya kwa kushtukiza uitwao ‘Acha Nikae Kimya.’ Wimbo unazungumzia masuala mengi yanayotokea sasa ikiwemo hofu iliyotanda baada ya Roma na wenzie kutekwa.
Wimbo huo hata hivyo umepokelewa kwa hisia tofauti.
Hizi ni sababu zake kwanini ameamua kuuachia:
Ili Nchi ipate maendeleo inahitaji Upendo na Ushirikiano wa Wananchi na Serikali..Na Nikiwa kama Msanii, jukumu langu ni kuhakikisha natumia Hekma na busara kukemea jambo nilionalo haliko sawa ili lirekebishwe, lakini pia panapokuwa hakuna maelewano jukumu langu pia ni kupatanisha ili kwa pamoja tujenge nchi yetu kusudi wazazi wetu, watoto pamoja na familia zetu waishi kwa Upendo Amani na kufurahia nchi yetu…Na ndiomaana kwenye nyimbo nakwambia “MI NA WEWE WA TAIFA MOJA…KAMBARAGE BABA MMOJA….SASA TOFAUTI ZA NINI TUSHIKAMANE TUKAIJENGE TANZANIA”… Unatakiwa utambue kuwa kila kiongozi ni Binadamu na kama wote tujuavyo, Binadamu hatujakamilika… hivyo katika nchi yoyote lazma wakati mwingine kuna jambo linaweza likawa haliko sawa, ila sisi kama wananchi tunatakiwa tutumie Hekima na Busara kwenye kufikisha ujumbe ama hoja zetu ili viongozi walieke sawa…Busara na Hekima itafanya viongozi watuelewe kirahisi na pengine mengi tuyatakayo tutimiziwe kirahisi… mfano mzuri, juzijuzi kupitia kipindi cha Clouds360 cha clouds Tv nlipopata bahati ya kuongea na Mh Raisi nilimuomba atufungulie Mabanda ya Chipsi na Bodaboda ziruhusiwe kufanyakazi hadi asubuhi maana zilikuwa nwisho saa 4 ama 5 usiku…kwakuwa nilitumia Hekima na busara kwenye Kufikisha hoja ama Ombi langu..alikubali na tukapewa ruksa na sasa hivi maeneo mengi ya Chipsi na Bodaboda yanafanya kazi hadi usiku mnene… hivyo tusikubali tu kulishwa Sumu za kuleta ugomvi kati yetu wenyewe kwa wenyewe eti Mara Tutukane mara sijui fanyeni hiki, wakati hata baadhi ya wanaochochea mambo hayo hawaishi Tanzania wanaishi Ulaya / Marekani / kifupi nje ya nchi…ikija kutokea bahati mbaya kimenuka wao watakuwa wanakula kuku kwa mrija huko walipo…halafu sisi na familia zetu ndio tutateseka na kuhaha kunusuru roho zetu usiku kucha.. Hatutaki makelele ya Uchonganishi mitandaoni, kama mtu kweli anauchungu na nchi na kweli akisemacho anamaanisha aje, na kwa pamoja twende sehemu husika kupeleka malalamiko sio kukaa kitandani kupost kuchochea Ugomvi kumbe anatuchora na kutufanya kama sie mataahira wake, anatupeleka mara kushoto mara kulia… Akikaa pekeake anatucheka kuwa sie wajinga wake katueka mkononi…